• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

KAMATI YA SIASA YA HALMASHAURI KUU YA CCM MKOA WA NJOMBE, IMEFANYA MAJUMUISHO YA ZIARA YA UKAGUZI WA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI KWA KIPINDI CHA KUANZIA MWAKA 2021 - 2023

Tarehe iliyowekwa: October 12th, 2023

Kamati ya Siasa Mkoa wa Njombe, ikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Njombe (MB), Mhe. Deo Sanga, Octoba 11,2023 ilifanya kikao cha majumuisho ya ziara iliyofanywa na kamati hiyo kwa siku tisa (9) kwenye Halmashauri zote zinaunda Mkoa wa Njombe.

Ziara hiyo ililenga kutembelea na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi CCM kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Mji Njombe na Makambako na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe,Makete,Ludewa na Wangingombe.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Njombe, Mhe. Deo Sanga, alisema kuwa katika ziara waliyoifanya  ambayo ilipitia kata 81 nakukagua miradi 81 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi Bilioni 43.601 ilikuwa ziara nzuri iliyowaonesha kazi kubwa na nzuri sana ambayo inafanywa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan kwenye sekta ya Afya ,Elimu,Miundombinu na Maji.

Pamoja na kazi nzuri iliyofanyika kwenye miradi iliyokaguliwa Mhe Sanga amesema, wamebaini changamoto kwenye baadhi ya maeneo nakutoa maelekezo kwa  watendaji wa Serikali  kupitia taasisi idara na vitengo kwenye halmashauri kuhakikisha zinafanyiwa kazi ili kuondoa malalamiko kwa wananchi.

"Tumegundua kuwepo kwa changamoto katika sekta ya Elimu na Afya hususani uwepo wa maboma ambayo ni viporo yanahitaji kukamilishwa na kuanza kutoa huduma , hivyo serikalini kupitia Halmashauri zote ziweke mkakati wa kukamilisha kwa haraka maboma hayo ili wananchi waweze  kuhudumiwa kiufasaha" Alisema Mhe Sanga.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Antony Mtaka, amewataka watendaji wote kwenye Halmashauri kuwajibika na kuhakikisha wanatoa kipaumbele kwenye miradi viporo hasa ile iliyoanzishwa muda mrefu ili ikamilishwe na kuanza kutoa huduma inayotakiwa .

Naye Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Pindi Chana , amewataka watumishi wote wa Serikali kutimiza wajibu wao kikamilifu sambamba na kutii sheria ili kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) sambamba na kutii sheria.

Kikao kazi hicho kiliwahusisha Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala Wilaya, Kamati ya Usalama ya Wilaya,  Wakurugenzi watendaji pamoja na zao, pamoja na wasimamizi wa Taasisi mbalimbali Serikali kutoka kwenye kila Wilaya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe