• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

KATIKA KUONGEZA UFANISI KATIKA UTENDAJI KAZI HALMASHAURI YA MJI NJOMBE IMEWAPATIA MAFUNZO WENYEVITI WA MITAA NA VIJIJI WOTE NDANI YA HALMASHAURI

Tarehe iliyowekwa: October 21st, 2022

Mnamo tarehe 21 Oktoba 2022,Halmashauri ya Mji Njombe kwa kushirikiana na Wakufunzi  kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI iliandaa mafunzo kwa Wenyeviti wote wa Mitaa na Vijiji ndani ya Halmashauri kwa lengo la kuwakumbusha majukumu yao pamoja kuongeza ufanisi katika utendaji wa majukumu yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa Mafunzo hayo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Kuruthum Sadick amewataka Wenyeviti kuhakikisha kuwa wanayatumia mafunzo hayo kurekebisha pale ambapo walikuwa wanakosea pamoja na kuongeza ufanisi zaidi kwenye utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Kuruthum alisema kuwa Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji ni kiungo muhimu katika maendeleo ya Halmashauri kwani wao ndio wenye watu na hivyo ni vyema kutumika vyema katika kuhakikisha jamii inakua na uelewa wa miradi inayotekelezwa katika Vijiji na Mitaa yao pamoja na kuwa washauri wema wa masuala mbalimbali wanayopelekewa mezani kwao badala ya kuwa wachochezi na wasababishi.

Akifungua mafunzo hayo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Erasto Mpete amewasihi Wenyeviti kuzingatia yale watakayokuwa wamefundishwa na kuyatumia mafundisho hayo kuleta mabadiliko chanya ndani ya Halmashauri na katika utendaji kazi.

Kwa upande  wake Mwenyekiti wa Mtaa wa National Housing  Malaki Mwandila amesema kuwa wanaishukuru Halmashauri kwa kuwaandalia mafunzo hayo ambayo yatawakumbusha wajibu wao na pia kuwaongezea ufanisi katika kuwahudumia Wananchi

Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Mji Njombe kupitia Idara ya Utumishi na Utawala imekua ikiandaa mafunzo kwa makundi mbalimbali ambapo awali yalifanyika mafunzo ya Madiwani kwa lengo la kuongeza ufanisi na kukumbusha wajibu na majukumu yao katika utekelezaji wa kazi zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe