• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Kituo cha Afya Ihalula sasa kuanza kutoa huduma za Mionzi

Tarehe iliyowekwa: November 9th, 2022

Katika kuadhimisha siku ya mionzi duniani Halmashauri ya Mji Njombe imezindua huduma za mionzi katika kituo cha Afya Ihalula jengo ambalo limegharimu kiasi cha shilingi milioni  92.6 ambapo Halmashauri imechangia kiasi cha shilingi milioni 90.6  na nguvu za Wananchi milioni 2.

Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa jengo la mionzi Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ihalula amesema kuwa kuanza kwa huduma hiyo ya mionzi kutapunguza gharama na umbali kwa Wananchi kutafuta huduma ya mionzi na jumla ya wakazi elfu kumi na mbili mia tisa tisini na nne (12,994) wanatarajiwa kunufaika na huduma ya mionzi katika kituo hicho.

Akizungumza na Wananchi waliofika kupata huduma katika Kituo cha Afya Ihalula Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Erasto Mpete  amesema kuwa kwa sasa huduma zote muhimu za ultra-sound, x-ray zimeanza kupatikana katika kituo hicho rasmi na hivyo hakuna haja ya kwenda katika vituo vya afya vingine kupata huduma hizo.

"Niwaombe Wananchi kutumia fursa ya kituo cha Afya Ihalula kuchangamkia fursa za kibiashara kwa kuanzisha maduka ya kisasa, hoteli na nyumba za kulala wageni ili Wananchi watakaokuja kupata huduma kituoni hapo wasikose malazi au huduma muhimu za madukani."Alisema Mpete 

Mwenyekiti wa huduma za Jamii Halmashauri ya Mji Njombe Angela Mwangeni ameishukuru Serikali kwa kusogeza huduma katika Kituo hicho ambacho awali Wananchi walilazimika kwenda Uwemba na Mjini Njombe kupata huduma za afya.Mwangeni amesema kuwa kwa sasa kazi iliyosalia ni kuhakikisha kuwa vituo hivyo vinatumika na pia kuweka matumaini kwa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa hatua kubwa waliyoifanya.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Kuruthum Sadick amewaahidi Wananchi kuwa atahakikisha kuwa anatafuta Wataalamu wa Chumba cha kuhifadhia maiti ili kuendelea kuimarisha huduma kituoni hapo na pia kupitia mapato ya ndani ya Halmasahuri kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa jenereta kubwa na la kisasa  litakalowezesha kuendesha shughuli zote kituoni hapo.Kwa upande wao baadhi ya Wananchi waliofika kupata huduma katika Kituo hicho akiwemo Benno Msemwa na Katarina Lupenza wamesema kuwa huduma zinazotolewa ni za kisasa na pia imewarahisishia kupunguza gharama za kusafiri na muda wa kutafuta huduma

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe