• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

LISHE BORA KWA WAJAWAZITO,ITASAIDIA KUPUNGUZA KUZALIWA WATOTO NJITI

Tarehe iliyowekwa: November 17th, 2024

Na,Ichikael Malisa. 


Jamii Mjini Njombe imehimizwa kuzingatia lishe bora na kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya zinaa haswa kwa wajawazito ili kukabiliana na changamoto ya watoto kuzaliwa kabla ya wakati(Njiti) na wenye uzito pungufu. 


Wito huo umetolewa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Dr. Jabil Juma,ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya watoto Njiti duniani yaliyofanyika Tarehe 17 Novemba 2024 katika hospitali ya Mji Njombe Kibena. 


Akizungumza na wazazi walioshiriki maadhimisho hayo Dr.Jabil alisisitiza umuhimu wa lishe bora kwa mama mjamzito na maandalizi sahihi kabla ya ujauzito. 


"Tuambizane ukweli , lishe duni kwa wajawazito ni moja ya sababu kuu zinazochangia kuzaliwa watoto njiti ,maandalizi ya kuzaa yanapaswa kuanza mapema, ndani ya umri wa kuzaa. Mama mjamzito anapaswa kuwa tayari na kuhakikisha anapata lishe bora kabla ya kushika ujauzito," alieleza.


Alionya pia juu ya athari za maambukizi ya magonjwa ya zinaa, kama vile kaswende na VVU, akieleza kuwa yanahatarisha afya ya mama na mtoto jambo ambalo linaweza kusababisha mtoto kuzaliwa kabla ya wakati na mwenye uzito pungufu. 


"Tukiamua kupambana na maambukizi haya kwa kujilinda na kuwa tayari kupima afya zetu mara kwa mara, itasaidia uzazi slama,  tunapata ujauzito tukiwa na afya bora na kuzaa watoto wenye afya njema," aliongeza. 


Aidha  aliwataka wananchi kuendelea kutoa maoni ya namna huduma za afya zinavyotolewa katika hospitali ili kusaidia maboresho na huduma bora kwa jamii. 


“Maoni yenu ni muhimu sana katika kuhakikisha tunaendelea kutoa huduma bora kwa jamii. Tutaendelea kuboresha mazingira yetu ili huduma hizi ziendelee kuwa bora.”


Maadhimisho ya siku ya watoto Njiti duniani 2024 yameongozwa na kaulimbiu inayosema, Kitendo kidogo,matokeo makubwa ikionesha umuhimu wa wazazi kutumia njia ya Kangaroo kusaidia ukuaji wa watoto Njiti.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe