• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MADIWANI HALMASHAURI YA MJI NJOMBE WAPIGWA MSASA

Tarehe iliyowekwa: October 19th, 2022

Halmashauri ya Mji Njombe Leo imeanza mafunzo ya siku mbili kwa Waheshimiwa Madiwani lengo ikiwa ni kuwajengea uwezo kwenye utendaji kazi wao na kuweza kutoa huduma nzuri kwa Wananchi kwa kuzingatia utawala bora wa sheria.

Akifungua mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Njombe Kissa Gwakisa ameipongeza Halmashauri kwa kuweza kuandaa mafunzo hayo na  amewataka Waheshimiwa Madiwani kuwa Wasikivu kwa kile watakacho fundishwa na Wakufunzi kwani kile kitakacho fundishwa ni muhimu sana kwao kwa sababu itawasaidia kufanya kazi zao za uongozi kwa weledi na kuwashirikisha Wataalam na Wananchi kwa ujumla.

“Niwapongeze kwa hatua hii na ni jambo jema la kuigwa na Halmashauri nyingine kutoa mafunzo kwa Madiwani.  Mafunzo ni jambo zuri kwani linatuongezea maarifa ya mambo mapya na pia kutukumbusha pale ambapo tulikuwa tumesahau. Tukumbuke kuwa kila Diwani atathaminiwa endapo atakua anatekeleza majukumu yake kwa weledi na ufanisi hivyo kwa yale yote ambayo yatakayofundishwa kupitia mafunzo hayo kila Diwani anapaswa kuyazingatia” Alisema Kissa

Awali  akitoa taarifa fupi ya lengo la mafunzo hayo  Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala Halmashauri ya Mji Njombe Ester Gama amesema kuwa ili kuwa na uelewa wa pamoja na kufanikisha uendeshaji wa shughuli za Halmashauri kwa ufanisi kati ya Waheshimiwa Madiwani na Watendaji ndio maana idara hiyo iliona umuhimu wa kuandaa mafunzo hayo  ambapo pia kwa siku ya ijumaa Halmashauri imeandaa mafunzo kwa  Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji vyote ndani ya Halmashauri ili kuweza  kukumbushana wajibu wao kwenye utekelezaji wa majukumu yao ya uongozi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Kuruthum Sadick amesema kuwa Halmashauri imeweza kufanikisha mafunzo hayo kwa kutumia rasilimali zake hivyo kila Diwani anatakiwa kuona umuhimu wa mafunzo hayo yatakayowezesha utendaji kazi wa ufanisi wa majukumu yao.

“Ili Halmashauri yetu iweze kuwa bora tunahitaji pia umoja na ushirikiano kuafnya kazi kwa kusaidiana na kukosoana pale ambapo tunakua tunakwenda tofauti ili wote twende pamoja. Mafunzo ni jambo moja lakini utekelezaji wa kile tulichojifunza ndio cha msingi na ambacho tunapaswa kukizingatia.”Alisema Mkurugenzi

Stephen Mutambi Mkurugenzi Msaidizi Utawala Bora na Maendeleo ya Jamii Ofisi ya Rais TAMISEMI ambaye ni miongoni mwa Wakufunzi wa Mafunzo hayo kwa Madiwani amesema kuwa ni vyema kila Diwani  kuhakikisha kuwa anakuwa na desturi ya kuwa na utawala wa kisheria ,kufanya kazi kwa uwazi na uadilifu na pia kuhakikisha Wananchi wake wanakua na taarifa sahihi juu ya masula mbalimbali  ikiwemo mapato na matumizi haya yote ikiwa ni kuwezesha utawala bora kwenye jamii wanayoihudumia.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti Diwani wa Viti Maalumu Kata ya Njombe Mjini Tumaini Mtewa amemshukuru Mkurugenzi na kuandaa mafunzo hayo ambayo yanawaongezea maarifa zaidi katika shughuli zao za uongozi na pia kuwakumbusha wajibu wao katika kuwahudumia Wananchi.

Tumaini aliendelea kusema kuwa mafunzo hayo pia yameweza kuwaeleza wajibu wao wa kuhakikisha kuwa wanaisemea Serikali na Wananchi  wanakuwa na uelewa wa shughuli zinazoendelea na zinazofanywa kwenye Kata zao.

“Mafunzo haya yamekuwa na umuhimu sana mfano kwa sasa katika kipindi hiki ambacho Halmashauri imepokea fedha za ujenzi wa madarasa hivyo ni jukumu leo kuhakikisha kuwa tunawaambia Wananchi” Alisema Tumaini

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Erasto Mpete amewashukuru Wakufunzi kuwa na mada ambazo moja kwa moja zinalenga kwenye utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na pia amesema kuwa yeye na timu ya Madiwani wa Halmashauri ya Mji Njombe wapo tayari kusikiliza na kutekelza yale yote yatakayokuwa yamefundishwa kwa muda wa siku mbili na kuyatumia kwa ustawi wa Halmashauri

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe