• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MASHAMBA YALIYOKUWA YANAMILIKIWA NA NJORECU KUPIMWA UPYA

Tarehe iliyowekwa: October 27th, 2022

Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya makazi Angelina Mabula ameagiza kuwa mashamba yaliyokuwa yamemilikishwa kwa Chama Cha Ushirika Mkoa wa Njombe (NJORECU) na baadaye Wananchi  kuyatumia mashamba hayo kuyaendeleza kwa muda mrefu, kufanyiwa upimaji upya na kukaa chini na pande zote mbili wakiwemo Wananchi wa Kijiji cha Ihanga na NJORECU ili kuona namna bora ya ugawaji wa maeneo hayo ambayo yatakuwa yamepimwa upya.

Awali akiwasilisha taarifa ya Kamati maalumu iliyoundwa kwa lengo la kutatua migogoro ya muingiliano wa kimatumizi katika Vijiji 975 Tanzania nzima Kijiji cha Ihanga Halmashauri ya Mji Njombe kikiwa ni miongoni mwa Vijiji vilivyofikiwa; Upendo Muguzi Mpima Ardhi kutoka Wizara ya Nyumba na Maendeleo ya Makazi  alisema kuwa,  Kamati hiyo ilibaini kuwa NJORECU walimilikishwa maeneo hayo tangu mwaka 1993 kwa barua ya Toleo na tangu kufanyika kwa umilikishwaji huo maeneo hayo hayakuwahi kuendelezwa  na Serikali ya Kijiji kuchukua uamuzi wa kuwagawia Wananchi.

Wakichangia katika nyakati tofauti tofauti baadhi ya Wajumbe wa Kamati hiyo na Viongozi kutoka Halmashauri ya Mji Njombe akiwemo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Filoteus Mligo, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Ester Gama amesema kuwa ni vyema  eneo hilo ambalo limebainika kuwa na ekari 244 tofauti na nyaraka za umiliki zinazoonyesha kuwa na ekari 392 sawa na ekari 968.5 kumilikishwa  kwa Wananchi wa Kijiji hicho kwani kwa muda mrefu NJORECU walilitelekeza bila kuliendeleza na hivyo kuwapasa kuomba eneo lingine kama nia yao inaendelea kuwepo.

Ziara hii ni mwendelezo wa ziara ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta kutembelea Nchi nzima na kutatua migogoro ambapo leo wamefika katika Mkoa wa Njombe ukiwa ni Mkoa wa 22 tangu kuanza kwa ziara hiyo.Mawaziri wanaoshiriki  ni kutoka katika wizara ya Nyumba na Maendeleo ya makazi Ikiwakilishwa na Waziri wa Wizara hiyo Angelina  Mabula, Wizara ya  Kilimo na Umwagiliaji  ikiwakilishwa na Naibu Waziri Antony Mavunde, Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikiwakilishwa na Naibu Waziri Abdallah Ulega , Wizara ya Maliasili na Utalii ikiwakilishwa na Naibu Waziri Mary Masanja, Ofisi ya Rais TAMISEMI ikiwakilishwa na Naibu Waziri David  Silinde , Ofisi ya Makamu wa Rais  Muungano na Mazingira ikiwakilishwa na Naibu Waziri Khamis Hamza Chillo na Wizara ya Maji ikiwakilishwa na  Naibu Waziri Mhandisi MaryPrisca Mahundi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe