Mgogoro wa Ardhi katika kijiji cha Itipula kilichopo kata ya Ihanga Halmashauri ya Mji Njombe uliodumu takribani miaka 20 baina ya familia ya Mkolwe,kanisa katoliki na Serikali ya Kijiji, Februari 15,2024 umefikia tamati baada ya timu ya wataalamu wakiongozwa na Afisa Tarafa Kata ya Igominyi,kuzungumza na pande zote tatu na kufikia maridhiano ya pamoja .
Walalamikaji wapande zote zilizokuwa na mgogoro katika maeneo hayo waliweza kufikia tamati ya kuyaacha maeneo ya shule na Kanisa baada ya mazungumzo ya pamoja na Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Mji Njombe Kanisia Mhagama ,Afisa Ardhi Ayubu Unduru pamoja na Baraza la ardhi la kijiji.
Aidha upande wa Familia ya Mkolwe,Serikali na Kigango cha Kanisa Katoliki Itipula walikubali kwa kauli moja kuwa maeneo yote ya shule yarudishwe katika ulimiki wa shule na eneo la kanisa lina baki kuwa la kanisa kwa makubaliano maalumu ambayo familia ya Mkolwe iliridhia kuondoa baadhi ya miti mikubwa iliyokuwepo katika eneo hilo na kuiacha ardhi pamoja na miti midogo iliyokuwepo.
Akifunga kikao hicho Afisa Tarafa kata ya Igominyi Nganyagwa Tumaini amewataka viongozi wa Kijiji hicho kuzingatia sheria za ardhi pamoja na kuzingatia nyaraka sahihi wakati wa kuuziana ardhi ili kuweza kuondokana na migogoro ambayo imekuwa ikileta chuki kwa wananchi.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe