• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MIAKA 60 YA MUUNGANO, NJOMBE YAPANDA MITI 1000 RAFIKI KWA MAZINGIRA

Tarehe iliyowekwa: April 26th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mheshimiwa Anthony Mtaka, Aprili 26,2024 ameshiriki pamoja na wananchi mkoani Njombe, kupanda miti 1000 aina ya mivengi kwenye bonde la Lunyanywi ikiwa ni siku  maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Akizungumza na wananchi walioshiriki maadhimisho hayo kwenye viwanja vya Halmashauri ya Mji Njombe, Mheshimiwa Mtaka  amewakumbusha wananchi wa Njombe umuhimu wa muungano.


"Muungano huu ni fahari yetu hatuna mama mwingine zaidi ya mama Tanzania,ni lazima tutembee tukiona ufahari wa muungano ambao ni kielezo na mfano kwa dunia, muungano wetu ni tunu muungano wetu ni lulu, tufanye kazi tukiamini nchi yetu ni moja ambayo ni Tanzania. "Alisema akinukuu hotuba ya Mhe. Rais aliyoitoa Aprili 25,2024.


Aidha aliwataka wananchi wa Njombe kuhakikisha wanaendelea kuhamasishana kupanda miti haswa miti ya matunda ili kuboresha lishe. 


" Wito wangu ningetamani kuona tunahamasika pia kupanda miti ya matunda kwenye familia na maeneo ya shule ili watoto waweze kula matunda kuanzia nyumbani na shuleni wakati wa chakula" 


Katika hatua nyingine alikemea vikali vitendo vya uchomaji moto kwenye misitu na mashamba ya miti. 


"Ni lazima tukemee tabia hizi za hovyo za visasi na hujuma kwa kuchoma mashamba ya miti, Mkoa wetu ni wa pili kwa upandaji wa miti, msisitizo wangu tujiepushe na vitendo vya  kuchoma moto mashamba, moto unakatisha tamaa kwa wawekezaji wapya, kilimo cha miti ni kilimo cha biashara, kinazalisha ajira, ni lazima tuulinde uchumi wa Mkoa wetu tukemee uchomaji  wa misitu."


Maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano  Mkoa wa Njombe yamefanyika Wilaya ya Njombe na kuhudhuria na wananchi pamoja wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa Njombe,Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Njombe Mji  na Makambako Mji pamoja na viongozi wengine wa kisiasa. 


Kaulimbiu ya maadhimisho ya siku ya muungano inasema "Tumeshikamana na Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa letu."


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe