• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Milioni 368 zawanufaisha Vikundi vya Wanawake Vijana na Walemavu Njombe

Tarehe iliyowekwa: March 4th, 2022

Halmashauri ya Mji Njombe imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 368,550,000/= kwa vikundi 34 vya wanawake vijana na walemavu katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2021/2022 huku shughuli kubwa za wanavikundi hao zikiwa ni kilimo, ufugaji ufundi ushonaji, kuosha magari, uokaji na biashara za duka.

Akiwasilisha taarifa fupi ya utoaji wa mikopo hiyo Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mji Njombe Bi. Enembora Lema amesema kuwa vikundi 34 viliweza kutembelewa na kukidhi vigezo, ambapo vikundi  10 vya wanawake vimepatiwa mkopo wa shilingi milioni 136, vikundi 18 vijana mkopo wa shilingi milioni 208 laki 7 na 6 watu wenye ulemavu kiasi cha shilingi milioni 23 na laki 8.

“Niwapongeze sana wanavikundi wa Njombe. Asilimia kubwa ni wakopaji na warejeshaji. Kuna maeneo mengi watu wanahangaika kwenye urejeshaji wa mikopo hii ila kwa Njombe mmekuwa warejeshaji wazuri. Niwaombe sasa mkasimamie miradi ili iwe endelevu.”Alisema Afisa Maendeleo ya Jamii.

Akizungumza katika hafla ya utoaji wa mikopo hiyo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe. Erasto Mpete amesema kuwa hali ya utoaji mikopo katika Halmashauri imeendelea kuimarika mwaka hadi mwaka na hii inatokana na namna Halmashauri ilivyojipanga katika zoezi zima la uchangiaji wa mapato na namna elimu ya ulipaji kodi ilivyowafikia Wananchi Mjini Njombe.

“Niwaombe sana mikopo mliyopatiwa ikatumike kwa matumizi yaliyoombewa kwani kukiuka vigezo hivyo mnakwenda kinyume na sheria na kanuni za utoaji mikopo kwani kikundi kitakuwa kimepoteza sifa ya ukopaji. Mikopo hii inatakiwa pia iwasaidie na wengine hivyo niwaombe Idara ya Maendeleo ya Jamii  kufuatilia mikopo hii ili mfuko uwe endelevu” Alisema Mpete.

Baadhi ya Taasisi zilizoshiriki kutoa elimu mbalimbali kwa wanavikundi hao zimefurahishwa na muitikio wa Wananchi kuchangamkia fursa hiyo na kuwataka Wananchi wanaolalamika kuacha na badala yake kutumia fursa ya mikopo ya Halmashauri kupata mitaji ya kuendeshea shughuli za ujasiriamali na kiuchumi.

Mwakilishi kutoka Taasisi ya Kupambana na rushwa TAKUKURU Daniel Mntambo amesema kuwa lengo la wao kushiriki katika hafla hiyo ya utoaji mikopo ni kuhakikisha kuwa hakuna viashiria vyovyote vya rushwa vinavyokuwepo katika zoezi zima la utoaji mikopo.Aidha Taasisi nyingine zilizoweza kushiriki na kutoa elimu kwa wanavikundi hao ni pamoja na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani, ofisi ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Njombe na Ofisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU.

Baadhi ya Wawakilishi kutoka katika makundi mbalimbali ambao ndio wanufaika wa mikopo hiyo likiwemo kundi la Walemavu Angela Kilasi,Herman Sanga mwakilishi wa Vijana na Grace Mbwilo kwa upande wa Wanawake amesema kuwa anaipongeza Serikali kwa kuweza kufikia makundi mbalimbali ya wahitaji.

“Naipongeza Serikali kwa kuweza kutoa mikopo mpaka kwa sisi Walemavu.Walemavu  wengi wapo  ila wamejificha hawatoki kwa sababu hawana vitu vya kuwatoa ndani. Ila kupitia sisi tunaopata mikopo naamini wengi watakwenda kutoka na tutakwenda kuwa mabalozi kuwa mikopo kwa walemavu inawezekana.”Alisema Angela Kilasi mwakilishi wa Walemavu

Halmashauri ya Mji Njombe imeendelea kutekeleza maagizo ya Serikali na kutekelza sheria ya fedha ya Serikali za Mitaa kifungu cha 37(A) ambayo inazitaka Halmashauri kutenga asilimia kumi ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kusaidia vikundi vya Wanawake,Vijana na Walemavu kwa kutoa mikopo isiyo na riba.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe