• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Milioni 97 Mapato ya ndani ya Halmashauri zatumika kununua Samani Miradi ya Afya na Elimu

Tarehe iliyowekwa: March 9th, 2021

Katika kuboresha mazingira ya upatikanaji wa elimu bora kwa wanafunzi na uwepo wa mazingira rafiki ya utoaji wa huduma bora za afya, Halmashauri ya Mji Njombe kupitia mapato ya ndani Halmashauri imechangia  kiasi cha Shilingi Milioni 97 laki 4 kwa ajili ya ununuzi wa samani katika Shule  7 za Sekondari na Zahanati mpya 5.

Akisoma taarifa ya hali ya utekelezaji wa mpango wa utengenezaji madawati kwa Shule za Sekondari zoezi lililoanza kufanyika mwezi Desemba 2020 mpaka sasa, Afisa Elimu Sekondari Procheus Nguli amesema kuwa licha ya Halmashauri kuendelea kutekeleza miradi mingine mpango wa kutengeneza madawati 775 ulifuatia uwepo wa Shule mpya ya Utalingolo na Kibena zilizoanza rasmi mwaka huu 2021 jambo lililopelekea ongezeko la uhitaji wa samani na kukidhi mahitaji ya samani katika shule nyingine za Sekondari zilizokuwa na uhitaji.

“Tulifanikiwa kutengeneza madawati 320 ambayo yameanza kutumika katika Shule mpya mbili ambazo ni Shule ya Sekondari Utalingolo na Shule ya Sekondari Kibena.Sekondari nyingine zitakazopatiwa samani hizo ni  Shule ya Sekondari Matola madawati 160,Uliwa 105,Mgola 90,Kifanya 80 na Viziwi madawati 20.”Alisema Nguli

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri Dkt. Yesaya Mwasubila amesema kuwa Halmashauri imeweza kununua meza 35, viti 65, makabati 10,na rafu 10 na viti vya aluminium 15 vifaa vilivyogharimu  kiasi cha shilingi milioni 35 laki 4.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Romanus Mayemba amesema kuwa zoezi la utoaji huduma kwa Wananchi ni zoezi endelevu na amewaomba wote waliokabidhiwa samani hizo kwa upande wa afya na elimu kuhakikisha utunzaji wake ili ziweze kuwa na manufaa hata kwa baadaye.

“Tunapotoa huduma ni vyema kutambua kuwa kuna fedha ya Serikali na michango ya Wananchi iliyotumika kununua vifaa hivyo.Halmashauri itaendelea kutoa huduma hizi kadri ambavyo Mwenyezi Mungu atakuwa amejalia lakini pia niwasihi Wananchi kuendelea kuchangia mapato ya Halmashauri na kusimamia mapato kwenye maeneo yao na kama kunaupotevu wowote tupeane taarifa kwani mapato haya ndio yanasaidia kupata huduma kama hizi na hatimaye kuleta maendeleo kwenye maeneo yetu”Alisema Mwenyekiti wa Halmashauri.

Akipokea samani hizo kwa niaba ya Wakuu wa Shule zitakazonufaika,Mkuu wa Shule ya Sekondari Uliwa Robert Emmanuel amesema kuwa anaipongeza Halmashauri kwa jitihada kubwa ambayo imekuwa ikionesha katika kutekelza miradi yake kupitia mapato ya ndani na ameahidi kuendelea kusimamia ufaulu katika shule  kwani Halmashauri imekua na msaada mkubwa kwao na fadhila pekee ni kuhakikisha Halmashauri inakuwa na kiwango kikubwa cha ufaulu katika ngazi za kitaifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe