• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MITAMBA BORA KITULO IPO

Tarehe iliyowekwa: October 28th, 2023

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe Ndugu Anthony Mtaka amewakaribisha watanzania wote wanaohitaji kufuga ngo'mbe wa maziwa, kufika kwenye Shamba la ngo'mbe kitulo lililopo wilaya ya makete mkoani Njombe kupata mitamba bora. 

Mhe. Mtaka amesema hayo Oktoba 28,2023 wakati wa kukabidhi zawadi ya Mkoa kwa Mheshimiwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Isdor Mpango, aliyekuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha maonesho ya Shirika la kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) kitaifa Mkoani Njombe.

Amesema kuwa mkoa wa Njombe umetoa  zawadi ya mitamba miwili yenye mimba kutoka Shamba la ngo'mbe kitulo ikiwa ni heshima kwa Mhe makamu wa Rais na habari njema kwa watanzania wote wafahamu kuwa, shamba la kitulo limefufuliwa na linazalisha mitamba bora yenye uwezo wa kutoa mpaka lita 30 za maziwa kwa siku.

"Mheshimiwa makamu wa Rais, kuna wakati wafugaji walilazimika kwenda mpaka Afrika kusini kununua ngo'mbe  bora kutokana na shamba letu  kuyumba, tunaamini kwa zawadi hii wewe mwenyewe utakuwa shahidi kwenye  uzalishaji wa maziwa" Alisema Mhe. Mtaka.

Katibu tawala wa Mkoa wa Njombe   Bi Judica Omari amekabidhi kamba zakufungia ngombe na mkoa utaratibu kusafirisha ngo'mbe hao hadi kufika nyumbani kwa Dkt Mpango. 

Zawadi nyingine iliyokabidhiwa kwa Mheshimiwa makamu wa Rais Dkt Mpango ni Kiwanja chenye hati kilichopo Halmashauri ya Mji Njombe iliyokabidhiwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe. Erasto Mpete, Pamoja miche ya karanga aina ya makademia. 

Akizungumza baada yakukabidhiwa zawadi hizo Mheshimiwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Isdor Mpango, ametoa shukrani kwa namna mkoa wa Njombe ulivyo mkarimu kwa kipindi chote alichofanya ziara  mkoani Njombe, nakuhidi kurudi tena Njombe kutembelea maeneo  ambayo hajafika. 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe