• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Mkuu wa Mkoa wa Njombe awasisitiza wenyeviti kuhimiza maadili na uadilifu katika uongozi

Tarehe iliyowekwa: February 14th, 2025

Njombe, 14 Februari 2025 – Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, amewataka Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa yote 463 ya mkoa huo kuwa mfano wa maadili mema na kuongoza kwa busara, hekima, na weredi ili kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi wao.


Akizungumza katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Mtaka alisisitiza kuwa uongozi ni dhamana inayohitaji uadilifu na uwajibikaji. Alieleza kuwa mwenyekiti wa kijiji au mtaa anapaswa kuwa kielelezo cha nidhamu, haki, na maamuzi sahihi yanayolenga kuimarisha ustawi wa jamii. Aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanazingatia misingi ya utawala bora kwa kushirikiana na wananchi katika kutatua changamoto zao.


"Uongozi unabeba sifa ya busara, hekima na weredi. Mwenyekiti anapaswa kuwa mfano wa maadili mema na mwelekeo sahihi kwa wananchi wake," alisema Mhe. Mtaka. Aliongeza kuwa viongozi wasiozingatia maadili wanapoteza imani ya wananchi na kushindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo. Mkutano huo ulihudhuriwa na Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa kutoka maeneo mbalimbali ya Njombe, ambapo walipata nafasi ya kujadili changamoto na mikakati ya kuboresha utendaji wao katika jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SIKU YA MAPOROMOKO YA MAJI

    June 16, 2025
  • SIKU YA MTOTO WA AFRIKA

    June 16, 2025
  • MHE. MTAKA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO, AIPONGEZA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE NA MAFUNDI.

    June 13, 2025
  • ELIMU KUHUSU UMILIKI WA ARDHI YATOLEWA KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA MFEREKE

    June 12, 2025
  • Angalia zote

Video

HUHITAJI TAKUKURU THAMANI YA FEDHA INAONEKANA -MHE. MTAKA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe