• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MKUU WA MKOA WA TANGA AFUNGA MASHINDANO YA SHIMISEMITA 2025

Tarehe iliyowekwa: August 30th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Batilda Burian, Agosti 29,2025 amefunga rasmi mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) 2025, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Mchengerwa.


Mashindano hayo yaliyoanza tarehe 15 Agosti na kumalizika tarehe 29 Agosti 2025, yameshirikisha Halmashauri 154 kati ya 184 zinazotarajiwa, huku yakihusisha zaidi ya watumishi 4,000 waliopambana katika michezo 15 tofauti.


Akizungumza wakati wa kufunga mashindano hayo, Mhe. Burian amewataka watumishi wa umma kuiga mshikamani na mshirikiano uliooneshwa kwenye michezo, hususan kuelekea uchaguzi ujao. “Siku ya uchaguzi siyo siku ya mapumziko, kila mtumishi anatakiwa kuwa mfano wa kuiga kwa kujitokeza kupiga kura kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu,” alisema.


Ameeleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameonesha dhamira thabiti ya kuimarisha sekta ya michezo nchini kwa kuwekeza kwenye miundombinu, hatua ambayo imewezesha wanamichezo kushiriki mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi.


Aidha amewasilisha maagizo ya Mhe.Mchengerwa ambaye, amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya michezo na kuwezesha ushiriki wa Halmashauri zote, na zile zenye changamoto za kifedha kuweza kushiriki michezo michache.Amesisitiza kuwa Halmashauri ambazo hazikufanya vizuri mwaka huu, zijipange mapema na kuendelea na mazoezi ya kila siku ili kujipatia ushindi katika mashindano yajayo.


Vilevile, ameitaka Kamati Tendaji ya SHIMISEMITA kufanya tathmini ya kina ili kuboresha zaidi mashindano yajayo na kuhakikisha yanakuwa bora na yenye ushiriki mpana zaidi.


Katika hafla hiyo Mhe.Batilda ametoa tuzo na zawadi kwa washindi mbalimbali katika mashindano hayo ambapo mshindi wa Jumla ni Halmashauri ya Jiji la Dodoma

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 15, 2025
  • MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA YASISITIZWA KWA WAKULIMA WA MTAA WA MPOBOTA - MJIMWEMA .

    October 11, 2025
  • MWEKEZAJI MADEBE AKABIDHIWA HATI MILIKI 16

    October 11, 2025
  • WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 11, 2025
  • Angalia zote

Video

IFAHAMU HUDUMA YA KIPEKEE INAYOPATIKANA NDANI YA SOKO KUU NJOMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe