• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MKUU WA WILAYA YA NJOMBE AAGIZA KUTUNZWA KWA KUMBUKUMBU ZA WAOMBAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10.

Tarehe iliyowekwa: September 1st, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Juma Sweda, amewataka Maafisa Maendeleo wa Halmashauri ya Mji Njombe kuhakikisha wanatunza kumbukumbu sahihi za waombaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri, ili kuepusha malalamiko kutoka kwa wananchi wanaokosa mikopo hiyo.


Mhe. Sweda ametoa agizo hilo Septemba 1, 2025, wakati wa hafla ya kukabidhi hundi za fedha na vitendea kazi kwa wanufaika wa mikopo hiyo. Amesema mikopo hiyo hutolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri, hivyo ni lazima kuzingatia uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wake.


“Ni muhimu kutunza kumbukumbu za waombaji wa mikopo, kwani hatua hii itasaidia kupunguza migogoro ambayo mara nyingi imekuwa ikiwalenga Maafisa Maendeleo na kudaiwa kupendelea. Ili kuepuka changamoto hiyo, ni vyema kuwe na kumbukumbu sahihi za waliowahi kuomba lakini hawakufanikiwa, ili katika awamu zinazofuata waweze kupewa kipaumbele,” alisema Mhe. Sweda.


Kwa upande wake, Afisa Maendeleo wa Halmashauri ya Mji Njombe, Bi. Enembora Lema, alisema kuwa kupitia tathmini iliyofanywa kuanzia ngazi ya Kata hadi Wilaya, jumla ya vikundi 94 vilikidhi vigezo vya kupata mikopo. Vikundi 34 vimepatiwa mkopo wenye thamani ya shilingi 1,518,196,000/= ambapo, vikundi 39 vya wanawake vimepatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi 637,540,000/=,vikundi 39 vya vijana vimepatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi 697,215,000/=na vikundi 16 vya watu wenye ulemavu vimepatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi 183,441,000/=


Mikopo hii ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri hutolewa kila robo mwaka kwa mujibu wa sheria, ikiwa na lengo la kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ELIMU YA WATU WAZIMA IJIELEKEZE KWENYE MITAALA MIPYA.

    September 09, 2025
  • KUANZA KWA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA 2025

    September 09, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE AAGIZA KUTUNZWA KWA KUMBUKUMBU ZA WAOMBAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    September 01, 2025
  • WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA NJOMBE TC

    September 01, 2025
  • Angalia zote

Video

ZIFAHAMU FAIDA ZA HERENI YA KIELEKTRONIKI KWA NG'OMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe