• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MNAODAI NJOCOBA, FIDIA BIMA YA AMANA INATOLEWA TCB BENKI

Tarehe iliyowekwa: May 22nd, 2024

Wateja ambao hawajachukua fidia ya bima ya amana baada ya kufungwa kwa iliyokuwa Benki ya Wananchi ya Njombe (NJOCOBA) Januari 2018 ,wametakiwa kufika kwenye tawi la Benki ya Biashara ya taifa (TCB) zamani Benki ya Posta wakiwa na kitambulisho cha taifa (NIDA) ili kufanyiwa uhakiki kwa ajili ya kulipwa stahiki zao.

Wito huo umetolewa Mei 22,2024  na  Joyce Shala Ofisa rasilimali watu mwandamizi wa Bodi ya Bima ya Amana (DIB) kwenye semina ya siku moja kwa wadau wa Bodi hiyo kutoka Wilaya ya Njombe iliyolenga kutoa elimu kuhusu Bodi ya Bima ya Amana, majukumu yake na kutoa taarifa masuala ya ufilisi wa iliyokuwa Benki ya wananchi ya Njombe (NJOCOBA).

“Tunawaomba wale wote waliokuwa wateja wa NJOCOBA ambao hawajalipwa fidia wafike kwenye tawi lolote la Benki ya biashara ya taifa(TCB) ,watafanyiwa uhakiki na kupatiwa stahiki zao, NJOCOBA ilikuwa na jumla ya wateja 12,323 tayari tumelipa wateja 4,014 madai yao yaliyokuwa na thamani ya shilingi  bilioni 1.2 sawa na asilimia 87 ya madai yote ,wateja ambao bado hawajalipwa madai yao ni 8,309 yenye thamani jumla ya shilingi milioni 189.”Alisema Bi.Joyce Shala.

Aidha Bi.Joyce amesema kuwa Bodi ya Bima ya Amana inaendelea na ufuatiliaji wa madeni ambayo hayajalipwa kutoka kwa waliokuwa wateja kwenye Benki ya wananchi ya Njombe (NJOCOBA).

“Tuna fanya kazi na mkusanya madeni anapita kwa wadaiwa,orodha tunayo na dhamana walizoweka tunayo na kwa takwimu za machi 2024 tunadai zaidi ya milioni 431 tunawakumbusha waweze kulipa madeni hayo.”Alisema

Bodi ya Bima ya Amana (DIB) tarehe 23 na 24 Mei 2024 itaendelea kutoa elimu kwa kuwatembelea wajasiriamali wadogowadogo walioko masokoni ,vituo vya pikipiki na maeneo mengine ndani ya Halmashauri tatu za wilaya ya Njombe ambazo ni Halmashauri ya Mji Njombe ,Halmashauri ya Mji Makambako na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe