• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MRADI WA KIZAZI HODARI MKOANI NJOMBE WAFANIKIWA KUWAFIKIA WANUFAIKA 25,097.

Tarehe iliyowekwa: September 29th, 2023

Na Ichikael Malisa

Mradi wa kizazi hodari kanda ya kusini Septemba 29,2023 umefanya uzinduzi wa  jukwaa la wadau wa ustawi wa mtoto mkoa wa njombe.

Mradi wa kizazi hodari kanda ya kusini ni mradi unaolenga kuimarisha afya, ustawi na ulinzi wa watoto yatima, wenye mazingira hatarishi pamoja na vijana wa rika balehe wanaoishi katika jamii zilizoathirika zaidi na maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Akielezea mafanikio ya mradi huo kwa kipindi cha kuanzia mwezi Octoba 2022  hadi Septemba 2023 Mkurugenzi wa  mradi huo Ndg Dorothy Matoyo amesema , mradi umefanikiwa kufikia wanufaika 25,097 katika mkoa wa Njombe na kati ya wanuafika hao  watoto ni 316,702 na walezi ni 8,395.  Kati yao 2,721 ni watoto na vijana wa rika balehe wanaoishi na virusi vya UKIMWI (VVU), ambao ni sawwa na  asilimia 16% ya  wanufaika wote.

Uzinduzi wa jukwaa hilo unalenga kuwashirikisha wadau mbalimbali baadhi ya changamoto ambazo mradi huu umekutana nazo ili kupata msaada wa wadau kufikia watoto wote katika huduma mbalimbali ikiwemo uhakika wa matibabu pale wanapougua pamoja ,elimu na kuwawezesha ili waweze kujikwamua badala yakutegemea msaada pekee.

“Ili kuhakikisha uendelevu wa huduma, tunahitaji kuwa na fungu maalumu kwa ajili ya kuwawezesha walezi na vijana wenye mawazo mazuri ya biashara ili waweze kujikwamua na kuwa msaada endelevu kwa kaya zao”

Baadhi ya changamoto zilizobainishwa na mradi wa kizazi hodari ni pamoja na watoto wengi kuishi kwenye nyumba zenye mazingira duni sana, Vijana wa umri wa miaka 15-18 kutokuwa shuleni, wananfunzi waliopo shuleni kukosa mahitaji muhimu kama sare, mabegi, viatu, na vifaa vya shule pamoja na mabinti wa rika balehe walio mashuleni kuhitaji msaada kuendelea kubaki shuleni kwa kupatiwa hifadhi salama wakati wa hedhi.

Aidha mkurugenzi wa mradi huo amesema wanahitaji msaada zaidi kwenye upande wa afya na kwamba kwa kuanza mradi umeweza kulipa kiasi cha shilingi 38,370,000/= kwa ajili ya kuwezesha bima ya Afya ya Jamii kwa Kaya 1,279 zenye jumla watoto 2,128 kwa kipindi cha kuanzia Septamba 2023 hadi Septamba 2024

“Pamoja na kuwa mradi umegharamia bima ya afya, hii ni sawa na asilimia 13% tu watoto walio kwenye mradi. Tunahitaji msaada wa wadau kufikia watoto wote ili waweze kupata uhakika wa matibabu pale wanapougua.”

Mradi wa kizazi kipya unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), kupitia mfuko maalum wa dharura wa kupambana na UKIMWI wa Raisi wa Marekani (PEPFAR), na unatekelwa na Deloitte kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Wizara ya Mandeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake Na Makundi Maalum ili kuhakisha mapambano dhidi ya virusi vya ukimwi yanafanikiwa.

Mradi wa kizazi hodari Mkoani Njombe unatekelezwa katika Halmashauri zote sita ambazo ni Halmashauri ya wilaya ya Njombe Halmashauri ya Mji Njombe,Halmashauri ya Mji Makambako,Halmashauri ya wilaya ya  Makete,Halmashauri ya wilaya ya Wanging’ombe na  Halmashauri ya wilya ya  Ludewa.

Wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa taasisi na mashirika yasiyo ya kiserikali walishiriki uzinduzi huo wa jukwaa la ustawi wa mtoto kwa mkoa wa Njombe.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe