• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Muda na Ubora Ukamilishaji Miradi uzingatiwe

Tarehe iliyowekwa: December 14th, 2021

Ziara  ya wajumbe wa Kamati ya fedha Halmashauri ya Mji Njombe ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Erasto Mpete ambapo  walitembelea na kukagua miradi inayotekelezwa katika Halmashauri ambapo chanzo cha fedha za miradi hiyo ikiwa ni Mpango wa mapambano dhidi ya UVIKO, nguvu za Wananchi na mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akizungumza katika ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Erasro Mpete amesema kuwa anaishukuru Serikali kwa kuipatia Halmashauri kiasi cha   Shilingi milioni mia saba arobaini kufanikisha ujenzi wa vyumba 37 vya madarasa katika Shule 12 za Sekondari.

Wakisoma taarifa za utekelezaji wa miradi hiyo mara baada ya kutembelewa na Wajumbe wa Kamati hiyo Mkuu wa Shule ya Sekondari Matola Gidion Massawe na Mkuu wa Shule ya Anne Makinda Veronica Mlozi  ambapo shule zao zinatekeleza ujenzi wa miradi ya madarasa kupitia fedha za UVIKO wamesema kuwa changamoto kuu iliyosababisha ucheleweshaji wa miradi hiyo imekuwa ni Uhaba wa Saruji.

Nao baadhi ya Wajumbe wa Kamati hiyo wakiwemo Ultrick Msemwa Diwani wa Kata ya Luponde, Honolatus Mgaya Diwani wa Kata ya Makowo na Filoteus Mligo Diwani wa Kata ya Lugenge wametaka miradi hiyo isimamiwe kikamilifu ili iweze kukamilika kwa wakati lakini pia kuwa na ubora uliokusudiwa.

“Madarasa yaliyojengwa yatasaidia sana kutatua upungufu wa vyumba vya madarasa tuliokuwa nao. .Januari tunatarajia kupokea wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza na kwa taarifa ambapo tumezipata katika shule tulizopita inaonyesha kuwa hatutakuwa na upungufu wa madarasa.Pia kwa hatua hii Wananchi wamepunguziwa mzigo wa kuchangia.Tunaipongeza Serikali kwa hatua hii.Alisema Mheshimiwa Msemwa Diwani wa Kata ya Luponde.

Katika shule ya Sekondari Yakobi, Shule inayotekeleza ujenzi wa vyumba 06 vya madarasa kwa ajili ya kidato cha tano, na ujenzi wa bwalo  la Wanafunzi ambapo Shule hiyo imeweza kuchangia zaidi ya shilingi milioni 15 ikiwa ni fedha za Elimu ya Kujitegemea(EK). Mkuu wa Shule ya Yakobi Editha John amesema fedha za EK zimekuwa na msaada mkubwa kwani Wazazi na Uongozi wa Shule wamekuwa na makubaliano kuchangia mawe na na nyaya za umeme kwa mwanafunzi yeyote atakayesababisha utovu wa nidhamu shuleni hapo.

“Uongozi wa Shule na Wazazi tumekubaliana na hata kwenye fomu za kujiunga tumesema kuwa kwa mwanafunzi ambaye atafanya utovu wa nidhamu shuleni,Mzazi atawajibika kulipa lori moja  la mawe na nyaya za umeme bando moja jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limesaidia kufanikisha ujenzi wa miradi hiyo.Mfano tumepata tripu zaidi ya 45 za mawe kupitia mfumo huo”Alisema Mkuu wa Shule hiyo

“Huu ni ubunifu wa hali ya juu. Nikupongeze Mkuu wa Shule kwa ubunifu huu na nafikiri kuwa tunaweza kutumia mfumo huu kwa shule nyingine ndani ya Halmashauri.”Alisema Diwani wa Kata ya Lugenge Filoteus Mligo

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Thadei Luoga amesema kuwa atahakikisha kuwa Walezi wa Kata ambao ni Wakuu wa Idara na Vitengo vya Halmashauri wanaendelea kuisimamia miradi hiyo kwa ukaribu zaidi ili kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliokusudiwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe