Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Erasto Mpete ametembelea katika shule ambazo zinaendelea na ujenzi wa vyumba vya madarasa kupitia fedha kutoka Serikali kuu na kusisitizia juu ya ubora wa madarasa, ukamilishaji wa miradi kwa wakati na utunzaji wa kumbukumbu za miradi hiyo.
Mpete amesema kuwa licha ya kuwa ujenzi wa miradhi hiyo unatakiwa kukamilika ndani ya siku 75 toka tarehe ya kuanza ujenzi ambayo ni tarehe 1/10/2022 ubora wa mradi ni jambo la muhimu linalopaswa kuzingatiwa ili thamani ya fedha iliyotolewa iweze kuonekana.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti baadhi ya mafundi wanaofanya kazi za ujenzi katika madarasa hayo wameipongeza Serikali kwa hatua hiyo kwani kupitia miradi hiyo imewaongezea kipato na kutanua wigo wa ajira kwa vibarua wanaosaidia shughuli za ujenzi huo na kuahudi kuikamilisha kwa wakati.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Ramadhan Nickson Nganyange akizungumza kwa niaba ya Wananchi wa Kata ya Ramadhan wamemshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia fedha hizo ambazo katika Kata hiyo shule ya Sekondari Maheve imepatiwa vyumba viwili vya madarasa
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe