• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Kasi ya umaliziaji Stendi ya Mabasi Njombe yamfurahisha Naibu Waziri TAMISEMI

Tarehe iliyowekwa: April 26th, 2019

Ni ziara ya Naibu waziri TAMISEMI  Ndg. Joseph Kandege katika kusimamia kwa ukaribu  ukamilishaji wa ujenzi wa stendi mpya ya mabasi Njombe,  ikiwa ni jitihada za kuhakikisha agizo la Mheshimiwa Rais alilolitoa katika Ziara yake Mkoani Njombe la kukamilisha ujenzi wa stendi linatekelezwa kufikia tarehe 10 Mei.

Akizungumza mara baada ya kutembelea katika kila hatua ya mradi na kujiridhisha na  shughuli za ujenzi zinazoendelea, Kandege alisema kuwa ifikapo tarehe 10 Mei stendi hiyo ianze kutumika kwani kwa hatua iliyofikia sasa haoni sababu zitakazozuia kuendelea kutumilika kwa stendi hiyo.

 “Siamini kwamba kwa hatua hii ambayo stendi imefikia itazuia stendi kutumika. Hakuna namna ambavyo tunaweza kujadili agizo la Mheshimiwa Rais. Tuliomba siku 20 akatuongezea siku 10. Ifikapo tarehe 10 Mei naomba stendi ianze kutumika.”Kandege Alisema.

Aliendelea kusema

“Kwa kazi ambazo zimefanyika nawapongeza sana kwa kuonyesha ushirikiano mkubwa. Nilikuja kutizama kabla  hatujafika hatua kubwa  kama hii  na niliamini kwa ushirikiano inawezekana. Naomba tuendelee kuthibitisha kuikamisha stendi kama ambavyo Mheshimiwa Rais aliagiza. Ni vizuri mkaanza kuwatangazia wenye vyombo vya usafiri kuhusu matumizi rasmi ya stendi hii. Wanachi wa Njombe waliisubiria stendi hii kwa muda mrefu sana.”

Ruth Msafiri ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe ambaye yeye alisema kuwa anamshukuru Mheshimiwa Rais kwani kupitia maelekezo yake yamefanikisha stendi kufikia hatua ilipo na kuanza kutumika mapema zaidi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda ameishukuru Serikali kwa kuwapatia fedha za utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa stendi ya kisasa Njombe na ameahidi kutekeleza agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuanza kutumika mara moja ifikapo tarehe 10 Mei.

“Tumeanza kukutana na wadau mbalimbali kwa ajili ya kuweka utaratibu wa matumizi” Alisema Mwenda.

Kwa mujibu wa mratibu  wa mradi huo ambaye ni Meneja wa Tarura wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhandisi Rais Tembo, alisema kuwa shughuli kubwa ya ujenzi imekamilika na mpaka kufikia tarehe 10 Mei kazi kubwa itakuwa imefanyika na shughuli zitakazosalia hazitakwamisha kuanza kwa matumizi ya stendi hiyo kama ilivyoagizwa.

Kwa wakati huo huo Naibu Waziri Kandege pia alitembelea na kukagua maendeleo ya  ujenzi wa soko la kisasa  Njombe na kuipongeza Halmashauri kwa kuweza kuchagua miradi ya ujenzi wa soko na stendi

“Nina kila sababu ya kuishukuru na kuipongeza Halmashauri ya Njombe TC kwanza katika kuchagua miradi ipi wafanye. Kuna Halmashauri zingine wanachagua miradi ambayo hata hicho kiasi cha fedha zilizotumika ukiambiwa zitarudi unaanza kupata mashaka. Mradi wa Stendi hali kadhalika soko vitakuwa ni vyanzo vya uhakika  vya  Halmashauri kuingiza mapato.”

Kandege aliongezea kuwa licha ya Halmashauri kunufaika lakini pia kwa kasi ya ujenzi wananchi wanafarijika kwa kazi ambayo inafanyika na watafurahia hali ya kufanya biashara katika mazingira rafiki.

Kandege ametoa rai kwa Halmashauri zingine kupata fursa ya kufika Halmashauri ya Mji Njombe na Kutembelea  mradi wa ujenzi wa soko la kisasa na  utakapokamilika utakuwa ni miongoni mwa miradi mizuri na yenye ubora wa hali ya juu tofauti na maeneo mengine ambapo miradi kama hii inatekelezwa.

Ujenzi wa soko la kisasa Njombe unatokana na  mradi wa ujenzi wa stendi ambapo Halmashauri ililazimika kufanya mapitio ya gharama za ujenzi wa stendi ya mabasi na miundombinu iliyokuwa imependekezwa awali na kufanikiwa kupunguza baadhi ya miundombinu iliyotakiwa kujengwa katika mradi wa ujenzi wa kituo cha mabasi na hivyo kupelekea Halmashauri kuwa na ziada kubwa ya fedha kwa kulinganisha kiasi kilichopangwa kutumika na kile kilichopokelewa  na hivyo kupata fedha ambazo ziliwezesha kuanzisha ujenzi wa soko la kisasa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe