• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainabu Katimba,Agosti 23,2025 ameongoza ufunguzi wa mashindano ya 40 ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) mwaka 2025 na kutoa maagizo kadhaa kwa viongozi na washiriki wote

Tarehe iliyowekwa: August 23rd, 2025

Akizungumza katika Uwanja wa Mkwakwani, Jijini Tanga, Mhe. Katimba amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kote nchini kuhakikisha wanatenga fedha za kutosha katika vitengo vya utamaduni na michezo na kuhakikisha mgawanyo wa fedha za ruzuku kila mwezi utolewa kwa kitengo hicho kama ilivyo kwa idara nyingine,jambo ambalo litawawezesha watumishi kushiriki ipasavyo katika mashindano hayo ikiwa ni sehemu ya kujenga mshikamano na afya bora kwa watumishi.


Amebainisha kuwa mwaka huu Halmashauri 15 zimeshiriki akiwataka Wakurugenzi ambao hawajawaleta watumishi wao kuhakikisha wanawasilisha wachezaji kabla ya mashindano kuhitimishwa.Amesisitiza watumishi kuendelea kufanya mazoezi kwa afya na kuanzia mwakani Halmashauri zote zinatakiwa kushiriki bila kukosa.


“Watumishi wa serikali waendelee kufanya mazoezi kila siku ili kujenga afya na kuimarisha utendaji kazi"Alisema Mhe.Katimba.


Ametoa wito kwa washiriki kuhakikisha wanatoa elimu na kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi la upigaji kura kuchagua viongozi mbalimbali litakalofanyika Oktoba 29, 2025.


“Kama ilivyo kaulimbiu ya mashindano haya,huu ni mwaka wa uchaguzi, michezo hii ni jukwaa la kuhamasisha wananchi kujitokeza kupiga kura onesheni uzalendo kwa kuchagua viongozi bora watakaoiwezesha serikali kusonga mbele katika maendeleo ya michezo mbalimbali, sambamba na kulinda maslahi ya Taifa,” alisema Mhe. Katimba.


Pia amekumbusha kuwa mashindano haya ni kwa ajili ya watumishi pekee, akipiga marufuku kwa watu wasiokuwa watumishi (‘mamluki’) kushiriki. “Iwapo itabainika kuna Halmashauri imeruhusu wachezaji wasio watumishi, hatua kali zitachukuliwa kwa mujibu wa kanuni za shirikisho,” alisisitiza.


Mashindano ya mwaka huu yanaenda na kaulimbiu ya "Jitokeze kupiga kura kwa maendeleo ya Michezo " yamehusisha michezo mbalimbali 15 na maonesho ya sanaa yakilenga kukuza vipaji, mshikamano na afya kwa watumishi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 15, 2025
  • MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA YASISITIZWA KWA WAKULIMA WA MTAA WA MPOBOTA - MJIMWEMA .

    October 11, 2025
  • MWEKEZAJI MADEBE AKABIDHIWA HATI MILIKI 16

    October 11, 2025
  • WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 11, 2025
  • Angalia zote

Video

IFAHAMU HUDUMA YA KIPEKEE INAYOPATIKANA NDANI YA SOKO KUU NJOMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe