• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Namna ufugaji kuku unavyowainua wanufaika wa TASAF III Njombe

Tarehe iliyowekwa: October 31st, 2018

Anna Ndawala (57)  mkazi  wa Kijiji cha Igominyi Kata ya Yakobi ni miongoni mwa mifano mizuri ya namna TASAF III inavyowawezesha wananchi katika kuinua uchumi.

Bi Anna ambaye anapokea kiasi cha shilingi elfu 32,000/= kila baada ya miezi miwili aliingia kwenye mpango mwaka 2015. Mara baada ya kuingia kwenye Mpango Anna alianza shughuli za ufugaji kuku mwanzoni mwa mwaka 2017 na alianza na ufugaji wa kuku 10 wa mayai. Kwa mwaka 2017 Anna alibahatika kuuza vifaranga katika awamu mbili tofauti na kujipatia kipato cha shilingi laki nane.

              “Awamu ya kwanza niliuza vifaranga 120, awamu ya pili nikauza    vifaranga 56 fedha nilizopata zilinisaidia kufanya shughuli mbalimbali. Nilifanikiwa kununua mahitaji ya shule ya mjukuu wangu, nilinunua mbolea ya kukuzia mahindi na zilinisaidia katika matumizi mbalimbali ya nyumbani. Nilifanikiwa pia kukarabati nyumba yangu na kuweka sakafu kwenye chumba ninacholala pamoja na kusakafia choo.”Alisema Anna

Aidha amefafanua kuwa licha ya kuwepo na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa elimu ya kutosha juu ya mbinu za ufugaji bora na wakisasa kutoka kwa wataalamu wa mifugo na mbinu za kukabiliana na magonjwa lakini bado hajakata tamaa.

Sambamba na hilo Anna ameshauri ni vyema wasimamizi wa wanufaika wa mpango huu ambao ni wanakamati kuhakikisha wanawatembelea wanufaika mara kwa mara ili kukagua shughuli za maendeleo wanazofanya na kujiridhisha kwani wanufaika wengine wamekuwa si wakweli  kwani pindi wapokeapo fedha za ruzuku wamekuwa wakizitumia hovyo badala ya kuwekeza katika shughuli za kuwaongezea kipato.

Kwa upande wake Mjukuu wa Mnufaika huyo ambaye anasoma darasa la tano katika shule ya Msingi Igominyi Agape amesema kuwa tangu walipoingia kwenye mpango amekuwa hakosi mahitaji muhimu ya shule kama viatu, madaftari, na ameendelea kufurahia maisha kwani hata katika familia wameweza kuboresha mlo kwa kula Mayai na kitoweo cha Kuku mara kwa mara jambo ambalo halikuwahi kutokea awali.

Kwa sasa Anna ambaye ni mnufaika wa TASAF III anakuku wa kienyeji wapatao 30 wa mayai 200 na kwa siku hukusanya mayai 150 ambayo ni sawasawa na Tray 5 za mayai.

Kufikia mwezi desemba mwaka 2018 Anna amedhamiria kukuza shughuli za ufugaji kuku, kutoka kuku 200 waliopo sasa mpaka kufikia kuku 700 jambo ambalo linamfanya kuishukuru TASAF kwa manufaa aliyoyapata.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe