Halmashauri ya Mji Njombe inataraji kunufaika na uhusiano wa kirafiki kati ya Nchi ya Ujerumani Mji wa Miltenberg na Halmashauri ya Mji Njombe ambapo kiasi cha shilingi bilioni 4 kikitarajiwa kutolewa na Ujerumani kuwezesha ujenzi wa dampo kuu la kisasa.Mratibu wa programu hiyo ambaye ni Katibu Tawala Wilaya ya Njombe George Emmanuel amesema kuwa yapo maeneo mengi ambayo Halmashauri itaweza kunufaika kupitia urafiki huu endapo mradi utakaotekelezwa kwa mara ya kwanza utaakisi matumizi ya fedha na ubora wa mradi uliokubaliwa.
"Zipo Manispaa na Majiji ambayo yameanza kunufaika na mahusiano na Nchi mbalimbali. Jiji la Dar es Salaam wao walianza na kwa sasa wanapokea miradi yenye zaidi ya bilioni 12.Hii ni kutokana na kuwa kwa jinsi walivyopokea fedha na kufanya utekelezaji wa mradi ndivyo ambavyo walivyoongezewa fedha zaidi mpaka kufikia kiwango hicho.Tunavyofanya vizuri ndivyo ambavyo tunaongezewa fedha"Alisema Katibu Tawala
Kai Struber ni Mtaalamu wa mazingira na uhifadhi wa taka ambaye alisema kuwa Mji wao umepiga hatua kubwa hususani kwenye ukusanyaji na uhifadhi wa taka ambapo taka huanza kwa kutengenishwa kuanzia majumbani mpaka eneo la dampo kuu.Aidha amesema kuwa taka zinazozalishwa mara baada ya kutenganishwa hutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali,kutengeneza mbolea na kuzalisha umeme.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe