• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

NJOMBE YAANZA MKAKATI UJENZI WA VYUMBA 98 VYA MADARASA

Tarehe iliyowekwa: October 7th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony Mtaka leo amehitisha kikao maalumu kilichowahusisha  Watendaji na Viongozi mbalimbali Mkoani Njombe lengo kuu ikiwa kuweka mkakati wa ukamilishaji wa madarasa kabla ya  wakati na  kuwa na umiliki wa pamoja kwenye ujenzi wa vyumba vya madarasa kazi inayotakiwa kufanyika kwa muda wa siku 75.

Akitoa taarifa za mapokezi ya fedha Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Judica Omary amesema kuwa Mkoa wa Njombe umepokea kiasi cha Shilingi Bilioni 1.96 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 98 katika Mkoa fedha ambazo ni ziada ya bajeti na ambazo zimepokelewa nje ya bajeti ya mwaka 2022/2023.

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwani ametuondolea mzigo wa kwenda kuchangisha Wananchi ili kukamisha madarasa haya. Fedha tumeshaletewa na nina amini kuwa kazi haitatushinda kwani hata mwaka jana tuliweza kukamilisha kwa wakati.Hizi ni hela za ziada kwa hiyo inatakiwa tujipange vizuri ili tuweze kutekeleza yale yaliyo kwenye bajeti pamoja na haya ya ziada.Kazi zote zinatakiwa ziende kwa pamoja ili ifikapo mwezi desemba madarasa yote yawe yamekamilika” Alisema Katibu Tawala.

Wakitoa taarifa ya mpango kazi wa maandalizi ya awali ya namna ya  utekelezaji wa ujenzi  vyumba hivyo vya madarasa; Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Wang’ing’ombe Maryam Muhaji , Mkurugenzi wa Wilaya ya Makete William Makufwe , Mkurugenzi wa Wilaya ya Ludewa Sunday Deogratias, Mkurugenzi wa Wilaya ya Njombe Sharifa Nabalang’anya, Mkurugenzi wa Mji Makambako Kenneth Haule na Kaimu Mkurugenzi Halmashuri ya Mji Njombe Shigela Ganja wamesema kuwa mpaka sasa wapo tayari kuanza kazi na pia taratibu zote muhimu zimeshaanza kufanyika ikiwa ni pamoja na kupeleka maombi kwa ajili ya mapitio ya bajeti,kufufua kamati za ujenzi pamoja na kupeleka taarifa kwa  barua kwenda ngazi za chini wakiwemo Watendaji na Wakuu wa Shule pamoja na maeneo yote yenye miradi  kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi.

Deo Mwanyika Mbunge wa jimbo la Njombe Mjini na Deo Sanga Mbunge wa Jimbo la Makambako wamemshukuru Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa anayoifanya ya ujenzi wa vyumba vya madarasa jambo ambalo linawapunguzia Wananchi mzigo mzito wa uchangiaji na badala yake kuweka nguvu katika shughuli nyingine.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Njombe Jassel Mwamwala amesema kuwa majengo yatakayojengwa yazingatie ubora na pia amewataka viongozi wa Chama kuhakikisha kuwa ngazi zote za chama wanashirikiana na Watendaji bila migongano na kuhakikisha kuwa kumbukumbu zote muhimu za ujenzi zinatunzwa sahihi.

Antony Mtaka Mkuu wa Mkoa wa Njombe amesema kuwa dhamira yake kubwa ni kuhakikisha kila mtu anashiriki ipasavyo kwenye usimamizi wa miradi hii toka hatua za awali ili kushirikishana na kuweza kwenda kwenye utekelezaji kwa pamoja.

“Itakuwa ni jambo la kushangaza tunashindwa kumaliza madarasa na unapoteza kazi  na fedha zipo kwenye akaunti. Wakati mwingine tunapoteza thamani yetu na heshima zetu na baadaye kudharaulika kwa tama ndogondogo ambazo hazina manufaa. Jenga darasa zuri ambalo litakupa sifa. “Alisema Mtaka

Aliendelea kusema “Mkoa wa Njombe tumepatiwa Bilioni 1.96. Dhamira yetu ni kuwa Mkoa wa kwanza kukamilisha madarasa kwa wakati. Na ili kujitofautisha na wengine ndani ya siku 75 tunapokwenda kuanza utekelezaji wa kazi hii siku moja kabla ya maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani tuwe tumekamilisha madarasa yote. ”Alisema Mtaka

Katika hatua nyingine Mtaka amezitaka Timu za Menejimenti za Halmashauri kujipambanua, kuwa na mawazo tofauti zaidi juu ya matumizi ya asilimia 40 za maendeleo kwa kuwa na miradi ya kipekee na kitofauti badala ya kuwa na mawazo yaleyale yanayofanyika katika ngazi Vijiji na Kata.

Kwa upande wa Halmashauri ya Mji Njombe imepokea kiasi cha shilingi milioni 520 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 26 vya madarasa kazi ambayo ina kwenda kuanza mara moja.






Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe