• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

NJOMBE YAWASILISHA ANDIKO LA USAFI NA MAZINGIRA UJERUMANI

Tarehe iliyowekwa: October 25th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Njombe akiwa ameongozana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Erasto Mpete,Katibu Tawala Wilaya George  Emmanuel na Mkurugenzi wa Halmashuri ya Mji Njombe Kuruthum Sadick wamekutana na uongozi wa Mji rafiki wa Milternberg  Nchini ujerumani na wafadhili wa mradi rafiki wa mazingingira ujulikanao kama  “Climate Partnership” na kuwasilisha andiko kuhusu uboreshaji wa mazingira ya Mji wa Njombe kwa kuwezesha ujenzi wa dampo la kisasa na kuifanya Njombe kuwa safi na Kijani.

 Akiwasilisha andiko hilo Mjini Milternberg Ujerumani Katibu Tawala Wilaya ya Njombe George Emmanuel alisema kuwa kupitia ziara ambayo alishiriki awali iliyopelekea kuja na andiko hilo jambo la kipekee waliloweza kujifunza ni namna bora ya utenganishaji na uhifadhi taka kutoka kwa wazalishaji taka,ukusanyaji na uchakataji taka na kuzalisha bidhaa kama mbolea na umeme jambo ambalo wao wameliona linafaa kufanyika pia katika Mji wa Njombe na kuachana  na utaratibu unaotumika sasa wa kukusanya taka kwa pamoja na kupeleka dampo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Njombe Kissa Gwakisa akiwasilisha salamu za Serikali ya Tanzania amesema kuwa Serikali imekua ikihamasisha urafiki baina ya Nchi mbalimbali kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kujifunza, kutafuta wadau kwenye uwekezaji na pia kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo Nchini Tanzania ili kuiletea Nchi Maendeleo.

Kissa alisema kuwa Serikali ya Tanzania kupitia Filamu ya “THE ROYAL TOUR” mhusika mkuu akiwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Samia Suluhu Hassan iliandaliwa lengo ikiwa ni kuonesha vivutio mbalimbali vilivyopo Nchini, kuvitangaza na kuhamasisha Watalii kutoka Nchi mbalimbali duniani kuweza kuja Tanzania kutembelea vivutio hivyo vya kipekee na hivyo kuwataka kutumia fursa hiyo kuvitembelea vivutio hivyo.

Kuhusu usafi wa mazingira Kissa amesema kuwa Tanzania iliweka utaratibu wa kuhakikisha kuwa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi inatumika kwa shughuli za usafi ili kuendelea kuwajengea Wananchi utamaduni wa kufanya usafi na utunzaji  wa mazingira.

Mara baada ya kuwasilisha andiko hilo lililobeba ujumbe muhimu wa kuifanya Njombe kuwa safi na kijani matarajio ni Njombe kunufaika kwa kupata dampo kuu kubwa na la kisasa na pia Wananchi wake kujengewa uwezo wa njia bora za uhifadhi taka kwa kuzitenganisha kuanzia majumbani mpaka kufikia eneo la dampo zitakapokuwa zinachakatwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe