• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

PROGRAMU ZA MAZINGIRA ZILENGE KUELIMISHA JUU YA UHIFADHI WA TAKA KWA KUZITENGANISHA

Tarehe iliyowekwa: September 28th, 2022

Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Judica Omary amesema kuwa bado elimu zaidi inatakiwa kwa Wananchi juu ya namna bora ya uhifadhi wa taka kwa kuzitenganisha na kuachana na tabia ya kuhifadhi taka zote sehemu moja.

Akizungumza wakati alipokutana na ugeni kutoka Miltenberg Ujerumani ambao ni Mji rafiki na Halmashauri ya Mji Njombe, Judica amesema kuwa ni vyema elimu  ikaendelea kutolewa na Wananchi kujengewa uwezo juu ya umuhimu  wa utunzaji wa taka kwa kuzitengeanisha kwa kuanzia katika hatua za awali kwa Wanafunzi mashuleni ili kuweza kutumia maarifa hayo majumbani kwao kwani mabadiliko hayaanzi kwa mara moja bali huanza kidogo kidogo.

“Katika muda wa siku tano ambao mtakuwa hapa Mjini Njombe natumaini mtaona hali halisi tuliyo nayo, lakini kuweza kutoa maoni na ushauri wa namna bora ya kuweza kuboresha ukusanyaji na uhifadhi wa taka ngumu katika Mji wa Njombe. Ili kupitia mradi ambao utakaoanzishwa kuona ni kwa namna gani yale ambayo hayatafanikiwa kutekelezwa kutokana na ukubwa wake yaweze kuwa ni sehemu ya mradi utakaoweza kuanzishwa ili Mji wa Njombe uweze kuwa mfano  bora kwenye uhifadhi na utunzaji wa mazingira.”Alisema Judica

Katika hatua nyingine Judica amesema kuwa changamoto nyingine ni kuwa katika kipindi cha kiangazi kumekuwa na moto ya mara kwa mara inayosababisha kuungua kwa misitu na hivyo kupelekea uchafuzi wa mazingira ambapo licha ya kuwa Mkoa,Wilaya na Halmashauri zimeweka sheria   mbalimbali za usimamizi wa maandalizi ya mashamba ambapo bado Wanananchi wamekuwa na muitikio wa kulega lega kwenye utekelezaji wa sheria za uhifadhi na ulinzi wa mazingira






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI NJOMBE TC AAGANA NA TIMU ITAKAYOCHEZA SHIMISEMITA.

    August 12, 2025
  • LISHE NA AKIBA YA MAZAO YAHIMIZWA NANENANE.

    August 08, 2025
  • KHERI YA SIKUKUU YA WAKULIMA 88 2025.

    August 08, 2025
  • ELIMU YA UNYONYESHAJI YATOLEWA KWA WAKAZI WA LWANGU

    August 05, 2025
  • Angalia zote

Video

ZIFAHAMU FAIDA ZA HERENI YA KIELEKTRONIKI KWA NG'OMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe