• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

RC MTAKA AWACHARUKIA MAWAKALA JUU YA MBOLEA ZA RUZUKU

Tarehe iliyowekwa: September 15th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka amewaonya Mawakala wote wanaojihusisha na usambazaji wa mbolea ya ruzuku Mkoani Njombe kwa kutumia  mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa fedha kwa wakulima kuhujumu zoezi la ununuzi wa mbolea ya ruzuku kuacha mara moja tabia hiyo na kuheshimu biashara zao.

Mtaka amesema hayo katika kikao maalumu kufuatia kuwepo kwa malalamiko ya Wananchi juu ya uwepo wa hujuma katika zoezi zima la usambazaji mbolea ya ruzuku huku Serikali ikiwa imetoa kiasi cha shilingi bilioni 150 kupunguza makali ya mbolea kwa wakulima ili kila mkulima aweze kunufaika kupitia ruzuku hiyo.

“Upo mchezo ambao Mawakala mnaufanya wa kusajili wakulima hewa na kuwapatia fedha kiasi cha shilingi elfu kumi kumi. Hatutalipa hela Wakala hewa. Na kama yupo wakala humu anayewapatia wakulima fedha kiasi cha shilingi elfu kumi wajisajili majina ya uongo umeamua kuiingiza biashara yako shimoni. Umeamua kufanya biashara ya mbolea fanya kwa nidhamu na heshimu biashara yako. Hatutakubali nia njema ya Serikali, nia njema ya Mheshimiwa Rais ya kutoa mbolea ya ruzuku kwa lengo la kuwasaidia wakulima halafu mtu aje afanye mchezo kwenye mbolea hii.”Alisema Mtaka

Aliendelea kusema “Kama umejiandaa kufilisika fanya mchezo na mbolea ya ruzuku. Hautajijirikia mbolea ya ruzuku ya mwaka huu.Hii ni mbolea iliyotolewa na Serikali kwa lengo la kuwasaidi Wananchi wake. Kama kuna Wakala hapa aache mara moja. Kwenye hili hakuna rangi tutaacha kuona Mheshimiwa Rais amezungumzia suala la Mbolea ya ruzuku kwa mara ya kwanza akiwa Mbeya na kwa mara ya pili  amezungumzia katika Mkoa wa Njombe na Mheshimiwa Waziri sipo tayari kuona hujuma katika mbolea hiyo.”Alisema.

Wakizungumza katika nyakati tofauti tofauti baadhi ya wasambazaji wa mbolea  wamesema kuwa zipo changamoto kadha wa kadha zinazowakabili kwenye usambazaji wa mbolea hizo ikiwa ni pamoja na makampuni yanayoingiza mbolea Nchini  kushindwa kuchagua mawakala licha ya Mawakala hao kutuma maombi na pia upatikanaji wa mbolea  hizo umekuwa si wa kuridhisha na wengine kushindwa kutoa baadhi ya mbolea kwa Mawakala  hao.

Aidha Wadau  hao wameomba Wakala wa Usimamizi wa Mbolea Nchini NFRA kuhakikisha kuwa katika viwango vya ujazo wa mbolea za ruzuku kuwa na ujazo mdogo  ili kila Mkulima aweze kunufaika na pia kuongeza kasi ya usajili wa Wakulima hususani katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye msimu wa Kilimo ambapo mahitaji ya mbolea ni mengi.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Mbolea NFRA amesema kuwa kwa sasa NFRA imeboresha mfumo wa usajili wa wakulima kwenye zoezi hilo ambapo kwa sasa zoezi hilo linafanywa na Maafisa Ugani ngazi ya Wilaya huku malengo kwa siku ikiwa ni usajili wa wakulima 2000 kwenye mfumo.

Aidha kuhusu upatikananji wa mbolea za ruzuku kwa ujazo wa mdogo wa kilo 5 na kumi Mwakilishi huyo amesema kuwa jambo hilo nalo litaanza kupatikana kwenye mfumo siku za karibuni kutokana na kuwa wakulima wengi wamekuwa na maombi ya kupatiwa mbolea zenye ujazo huo.

Awali akiwasilisha taarifa ya usambazaji wa mbolea na uandiksihaji wa wakulima  katika Mkoa wa Njombe Afisa Kilimo Mkoa wa Njombe Joel amesema kuwa Mkoa umeweka malengo ya kuwasajili wakulima 214, 870 kwa Mkoa mzima ambapo wakulima walioandikishwa na kutambuliwa kwenye daftari ni wakulima 160,752 na waliosajiliwa kwenye mfumo tayari kwenda kuchukua mbolea ya ruzuku ni Wakulima 99,645 sawa na asilimia 46.5 na Wakulima waliokwisha pata mbolea ni Wakulima 11,682 sawa na asilimia 5 ya Wakulima waliokwisha pata mbolea.Huku  kiasi cha mbolea kilichokwisha pokelewa kikiwa ni tani  3556.8.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe