• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

REPSSI,TAMISEMI Watoa mafunzo ya huduma ya Kisaikolojia na Kijamii kwa kamati ya ulinzi wa Mwanamke na Mtoto

Tarehe iliyowekwa: April 22nd, 2021

Kamati ya ulinzi wa Mwanamke na Watoto katika Halmashauri ya Mji Njombe imepatiwa  mafunzo yaliyolenga kuboresha utoaji huduma ya kisaikolojia kwa jamii ili kuweza kukabiliana na majanga kikamilifu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mkurugenzi Mkazi kutoka shirika la REPSSI Edwick Mapalala amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwani makundi ya Wanawake na Watoto yamekuwa yakikabiliana na ukatili mkubwa ndani ya jamii huku kundi hilo likiwa ndio waathirika wakubwa zaidi.

Wakiwasilisha mada mbalimbali juu ya utoaji wa huduma ya kisaikolojia kwa makundi maalumu wawezeshaji wa mafunzo hayo wamesema kuwa katika vipindi vya majanga mfano milipuko ya magonjwa,vita,mafuriko wanawake,watoto,wazee na watu wenye ulemavu wamekuwa wakiathiriwa na majanga yanayotokea na hivyo kamati ya ulinzi na usalama wa mwanamke na mtoto inatakiwa kuhakikisha kuwa inakuwa na uelewa wa kutosha juu ya utoaji wa huduma ya kisaikolojia ili kuweza kujiandaa wakati  majanga yanapotokea.

Miongoni mwa mambo yaliyozua mjadala katika mafunzo hayo ni pamoja na sheria ya mtoto chini ya miaka 18 anapomfanyia ukatili wa kingono mtoto mwenzake ambapo mwalifu  huweza kupewa adhabu ya viboko au kulipa faini jambo linaloonekana kama ni uonevu kwa mtoto aliyefanyiwa  ukatili na wameiomba Serikali kuona ni kwa namna gani sheria ya mtoto chini ya miaka 18 inaweza kufanyiwa maboresho kwani kwa sasa mtoto wa chini ya miaka 18 anaweza anakuwa tayari amepevuka na anauwezo wa kumpa mimba mtoto mwenzie hivyo ni vyema umri ukapunguzwa na adhabu pia ikaongezwa tofauti na hali ilivyo sasa.

Mara baada ya kupatiwa mafunzo hayo, kamati iliweza kuandaa mpangokazi wa Halmashauri wa kutokomeza  ukatili dhidi ya wanawake na watoto ambapo  miongoni mwa majukumu ya kusimamia dhana muhimu zinazohusiana na ulinzi na usimamizi wa kamati ngazi ya Kata pia kamati itawatambua wadau mbalimbali ili kuweza kushirikiana katika kuleta nguvu ya pamoja na kutekeleza mipango ya ulinzi na utoaji wa msaada wa kisaikolojia na elimu kwa jamii  na hatimaye jamii iweze kuelimika na kutokomeza masuala ya  ukatili kikamilifu

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe