• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

"Sasa Tutafika Kona kwa Kona" Waratibu Elimu Halmashauri ya Mji Njombe

Tarehe iliyowekwa: July 27th, 2018

Halmashauri ya Mji Njombe imepokea jumla ya pikipiki 13 zenye thamani ya shilingi milioni 39 kwa waratibu elimu Kata 13 lengo ikiwa ni kufanya ufatiliaji na usimamizi wa elimu katika Kata.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Salum Mkuya amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuboresha sekta ya elimu kwa kuhakikisha kuwa wasimamizi wa elimu wanawezeshwa upatikanaji wa vitendea kazi ili kufanya mazingira ya kazi kuwa rafiki.

“Pikipiki hizi zikafanye kazi ya ufuatiliaji kwa kupandisha kiwango cha ufaulu, kuhakikisha wanafunzi wanajua kusoma na kuandika ikiwa ni sambamba na kuthibiti utoro mashuleni.”Alisema Mkuya

Aidha, Mkuya ameiomba Halmashauri kuhakikisha kuwa pikipiki zote zilizokabidhiwa zinapatiwa bima kama serikali ilivyoagiza.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri Edwin Mwanzinga amesema kuwa anaishukuru serikali ya CCM kupitia kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kwa kutambua umuhimu wa pikipiki hizo kwa waratibu elimu kwani itarahisisha shughuli za usimamizi na ufuatiliaji elimu hususani katika Halmashauri ambazo maeneo mengi jiografia yake ni ngumu kufikika kutokana na ukubwa wa eneo halikadhalika changamoto za miundombinu.

 “Najua waratibu mlikua mnafanya kazi katika mazingira magumu niwaombe sasa tukafanye kazi bila visingizio na ni lazima tuwe wa kwanza kimkoa kwa sababu tumepata vitendea kazi. Lakini niwaombe sana mkazitunze pikipiki hizi ili tuweze kwenda nazo kwa muda mrefu. Kwa wale ambao hamjui kuzitumia tusitumie pikipiki hizi kujifunzia. Ni imani yangu mtaenda kujifunza mpate leseni na muweze kuzitumia vizuri na kwa tahadhari” Mwanzinga alisema

Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya waratibu elimu Ester Mjuu Mratibu Elimu Kata ya Ramadhani Halmashauri ya Njombe alisema kuwa sasa wataweza kufika kila kona ya Kata zao katika kufuatilia usimamizi wa elimu.

“Tunashukuru sana kwa vitendea kazi hivi,miongoni mwa changamoto iliyokuwa inatukabili imepata ufumbuzi tutaenda kufanya kazi kwa kadri mlivyotuelekeza ili kuhakikisha kuwa tunakuwa na Taifa la wasomi kwa kufanya ufuatiliaji na usimamizi wa karibu kwenye sekta ya elimu.”Alisema

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe