• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

SERIKALI IMETOA MATREKA,TUNAHAMIA KWENYE KILIMO CHA KISASA

Tarehe iliyowekwa: December 21st, 2024

Kituo cha Rasilimali za Kilimo kilichopo kijiji cha Kisilo, kata ya Lugenge, Halmashauri ya Mji wa Njombe, ni miongoni mwa vituo vitakavyonufaika na matrekta mapya yaliyoletwa na Serikali kwa lengo la kusaidia wakulima kuhamia kwenye kilimo cha kisasa chenye tija.

Kauli hiyo imetolewa tarehe 21 Desemba 2024 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mheshimiwa Deo Philip Mwanyika, alipoongoza kamati hiyo kutembelea na kukagua rasilimali zilizopo  kituo hicho.

Mheshimiwa Mwanyika amesema Serikali inatambua mchango wa sekta ya kilimo kwa pato la taifa, na kwamba mbali na ruzuku ya mbolea na viuatilifu, sasa inatoa zana za kisasa, zikiwemo matrekta, ili wakulima wapate fursa yakukodisha kwa gharama nafuu.


"Nimefurahi kusikia namna kituo hiki kimewanufaisha watu wengi. Ni lazima tufanye maboresho. Wakulima sasa hamna haja ya kununua matrekta kwa gharama kubwa, kwani Serikali inatoa matrekta, na hapa Njombe tayari yamefika yatakuja hapa kisilo". alisema Mheshimiwa Mwanyika.


Kamati hiyo, kupitia mwenyekiti wake, ilitoa maelekezo ya kufanya maandalizi ya mapokezi ya matrekta hayo kwa kuhakikisha eneo hilo linawekewa uzio kwa ajili ya ulinzi wa zana hizo.


Kwa upande wao, wananchi wa kijiji cha Kisilo, akiwemo Kalo Mligo na Frank Mwabena, wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia kamati hiyo, kwa kutambua umuhimu wa vituo kama hivyo ambavyo vimekuwa msaada mkubwa kwa wakulima na wafugaji.


"Kituo hiki kimekuwa msaada mkubwa. Kupitia kituo hiki nilihamasika kufuga ng'ombe. Kinawasaidia wananchi wengi, siyo tu wa kijiji cha Kisilo, bali wa Halmashauri nzima kwa ujumla," alisema Frank Mwabena, mkazi wa Kisilo.


Kituo cha Zana za Kilimo cha Kisilo kilianzishwa mwaka 2003 chini ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine kwa lengo la kuibua na kueneza teknolojia mpya za kilimo kwa nadharia na vitendo. Kituo hiki kimewqsaidia wananchi kuzalisha mazao kama mahindi, ngano, viazi, na maharagwe, kwa kutumia zana bora za kilimo, huku  kikifanya tafiti na majaribio ya zana na mbegu bora ili kusaidia wakulima kutumia mbegu bora na kuondokana na matumizi ya jembe la mkono.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe