• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Serikali Yaendelea Kuimarisha sekta ya Elimu Nchini

Tarehe iliyowekwa: July 24th, 2018

Mkoa wa Njombe umepokea jumla ya vitabu elfu 30355 kwa ajili ya masomo ya Hisabati, Kiingereza, Kiswahili, Maarifa na Uraia huku Halmashauri ya Mji Njombe ikipatiwa jumla ya vitabu elfu 4634 ikiwa ni vitabu vya kiada kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la nne.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya vitabu hivyo yaliyofanyika katika Ofisi za Halmashauri ya Mji Njombe, mwakilishi wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Salum Mkuya alisema kuwa vitabu hivyo vinavyosambazwa Nchi nzima katika Halmashauri zote vinalenga kuimarisha sekta ya elimu kwa upande wa Shule za Msingi, kama ilivyoainishwa katika   Ilani ya CCM ya mwaka 2015-2020.

“Mtaona nyie wenyewe kwenye elimu bila malipo, fedha za uendeshaji, posho za wakuu wa shule na waratibu elimu kata, ujenzi wa madarasa na madawati haya yote yanafanywa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli hatuna budi kumuombea kwa mabadiliko haya anayofanya kwa kuandika historia ya Tanzania mpya na inaonesha ni kwa jinsi gani utekelezaji wa Ilani unafanyika kwa kasi kubwa.”Alisema Mkuya

Aidha, Mkuya amewaomba viongozi wa Mkoa, wasimamizi wa elimu katika ngazi za Halmashauri na waalimu  kuhakikisha kuwa vitabu hivyo vinatunzwa na vinatumika ipasavyo kwani ni haki ya watoto kupata elimu bora na serikali itaendelea kuboresha sekta ya elimu mpaka maendeleo yapatikane.

Akipokea vitabu hivyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi. Ruth Msafiri alisema kuwa amefurahishwa sana na upatikanaji wa vitabu hivyo na inaonesha waziwazi ni kwa jinsi gani Mhe. Rais anatekeleza ahadi zake kwa wakati  pindi anapotamka jambo.

Kwa wakati huo huo Mkuu huyo wa Wilaya Amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda kwa kusimamia vyema sekta ya elimu kwani Halmashauri ya Mji Njombe imekua ikiongoza Kimkoa katika mitihani ya Kitaifa kwa upande wa Shule za Msingi na Sekondari huku ufaulu wa Kimkoa ukiwa ni wa daraja A.

Antony Katani ni Katibu CCM Wilaya ambaye yeye amempongeza Rais kwa kutafsiri kwa vitendo utekelezaji wa ilani hususani kwenye sekta ya elimu kwa kuhakikisha uimarishaji wa sekta hiyo ikiwa ni sambamba na upatikanaji wa vitabu vya kutosha mashuleni.

Katani pia amewataka wale wote wanaobeza mpango wa serikali kutoa elimu bila malipo kupuuzwa kwani hawana nia njema na serikali ya awamu ya tano.

“Kwa Mtanzania yeyote mwenye nia njema na Nchi hii hapa ndipo tulipokuwa tunapahitaji,na tunaamini kuwa Mhe. Rais atatupeleka mahali ambapo wengi tulikuwa tunapahitaji. Wale wote wanaobeza jitihada za makusudi anazofanya Mhe. Rais kwa upande wa elimu bila malipo tuwapuuze na Mwenyezi Mungu awalaani” Alisema Katani

Nae mwakilishi wa wanafunzi kutoka shule ya Msingi Ruhuji B John Mwanyika ameishukuru serikali kwa kupatiwa vitabu hivyo na amesema kupitia vitabu hivyo walivyopokea leo vitawawezesha wao kusoma kwa bidii na wanaahidi kufanya vizuri katika masomo yao kwani tatizo la uhaba wa vitabu katika masomo yote sasa umepata ufumbuzi na kufikia kikomo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe