Halmashauri ya Mji Njombe inaungana na mataifa mengine Barani Afrika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika, ikiwa ni kumbukizi muhimu yenye lengo la kuhimiza ulinzi na ustawi wa watoto.
Kaulimbiu ya mwaka huu inasema “Haki za Mtoto; Tulipotoka, Tulipo na Tuendako” , ikihamasisha jamii kutafakari kwa kina kuhusu hali ya utekelezaji wa haki za watoto tangu kuanzishwa kwa Sera ya Maendeleo ya Mtoto mwaka 2008.
Lengo kuu la maadhimisho haya ni kuendelea kuelimisha na kuhamasisha jamii pamoja na wadau mbalimbali kutathmini mafanikio yaliyopatikana na changamoto zinazokwamisha utekelezaji wa haki za mtoto, huku wakijipanga kwa hatua madhubuti za kuboresha mazingira ya malezi na makuzi bora kwa watoto.
Kwa mujibu wa sera ya maendeleo ya mtoto ya mwaka 2008 kuna haki tano za msingi za mtoto ambazo ni:
• Haki ya Kuishi
• Haki ya Kuendelezwa
• Haki ya Kulindwa
• Haki ya Kushirikishwa
• Haki ya Kutobaguliwa
Haki hizi ni nguzo muhimu katika kuhakikisha mtoto anakua na kuendelezwa kwa afya njema, elimu bora, usalama, na usawa katika fursa zote za maisha.
Serikali, wazazi, walezi, jamii na wadau wa maendeleo wanahimizwa kushirikiana kwa dhati kulinda na kukuza haki hizi ili watoto wote waweze kukua katika mazingira salama, yenye upendo na fursa za kufikia ndoto zao.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe