• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

SIMAMIENI UKWELI WAKATI WAKUWAHUDUMIA WANANCHI.

Tarehe iliyowekwa: May 26th, 2024
  1. Naibu  Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe.Dkt.Doto Biteko amewataka wataalamu watakaofanya kazi yakutoa msaada wa kisheria kwa wananchi mkoani Njombe kuhakikisha wanasimamia ukweli kwenye huduma wanayoitoa. 

Dkt. Biteko amesema hayo Mei 26,2024 kwenye uzinduzi wa kampeni ya huduma ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaing) itakayofanya kazi kwa siku 10 katika Halmashauri 6 za Mkoa wa Njombe.


Aliwataka wananchi kuacha misimamo iliyopitiliza wakati timu ya mawakili itakapokuwa inawasikiliza na badala yake wafuate ukweli.

“Maandiko yanasema ukijua kweli itakuweka huru nawe utakuwa huru kweli kweli, mawakili simamieni ukweli mtapokuwa mnasikiliza watu hawa watakaokuja kwenu,”Alisema Dkt.Biteko.

Mhe.Biteko alibainisha nia ya Serikali kwenye kampeni hiyo ni kuwafikia wananchi haswa wale wasioweza kumudu gharama za kisheria katika utatuzi wa migogogro kwa njia mbadala nakutoa rai kwa wananchi kutumia vizuri fursa hiyo.

“ Niwaombe wananchi wa Tanzania kupitia kampeni hii,wale ambao hawawezi kumudu gharama za mawakili wachukue fursa hii kuwaona wataalamu wetu wa kisheria, waweze kusikilizwa nakupatiwa ushauri na hatimaye kumaliza migogoro hii”.Alisisitiza Dkt Biteko .

 Katika hatua nyingine alitoa wito kwa jamii kuwa na utamaduni wa kutoa taarifa na kutafuta msaada wa kisheria mapema ili migogoro inayoibuka kwenye jamii itatuliwe kabla yakuwa na madhara.

“Ili tuwe na jamii ambayo ina stahimiliana,jamii ambayo watu wake hawana  migogoro mingi, ni muhimu migogogro ikatatulia mapema ,tukisubiri watu wameapizana wamefika mbali ,hata hawa wataalamu wanaokuja huko watakuja kushughulika na kisasi badala yakutafuta suluhu”.Alisema.

Akihitimisha hotuba yake alitoa wito viongozi kwa viongozi wa Serikali kutoa ushirikiano kwa wataalamu watakaofanya kazi ngazi ya kata na vijiji ili kufanya kazi iwe rahisi na kutimiza lengo la kampeni hiyo.

Kauli mbiu ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaing) inasema Msaada wa Kisheria kwa Haki,Usawa,Amani na Maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe