• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

SIMAMIENI VIZURI FEDHA ZINAZOTOLEWA KWA AJILI YA MIRADI YA MAENDELEO

Tarehe iliyowekwa: April 18th, 2024

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ametoa wito kwa  watendaji wa ngazi mbalimbali za Serikali, kuwajibika na kusimamia vizuri fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya miradi ya mdeleo ili thamani ya fedha hizo ionekane. 


Dkt. Nchimbi  amesema hayo tarehe 18 Aprili, 2024 wakati akizungumza na wananchi mjini Makambako kwenye mkutano wa hadhara.

"Nimesikia hapa, Mkoa wa Njombe umepewa shilingi bilioni 900, nimesisimka kwasababu hizi ni hela nyingi sana,” alisema na kuongeza kuwa, “niwasisitize wafanyakazi wote wa Serikali kuwa waaminifu katika usimamizi wa fedha za miradi zinazotolewa na Serikali zitumike vizuri." 


Aidha, amevitaka vyombo vya usalama ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuisaidia Serikali kwa kuzuia wabadhilifu wa mali za umma na kufanya kazi ya kuzuia badala yakusubiri kukamata wahalifu.

 "TAKUKURU tusisubiri kukamata walioiba, tuzie wezi wa mali ya umma wabadhirifu na wala rushwa kwa kufuatilia fedha zinazotolewa katika miradi mikubwa tangu inapoanza.''


Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu huyo wa CCM, amewakumbusha wananchi wote kuwajibika kwa taifa lao kwa kuwa waadilifu na wazalendo. 

"Kila mmoja wenu ajitahidi kuwa mwema kwenye jamii, usiwe tapeli, usitoe rushwa, usiwe mwizi, lipende taifa lako, haya mambo yasiyofaa hayajengi nchi yetu, wote tuungane tuijenge Tanzania yetu, nchi yetu bado changa lakini inaweza kujengwa na Watanzania wakiamua kufanya mambo kwa kuipenda nchi yetu."


Ziara ya Katibu wa CCM  mkoani Njombe imenza Aprili 18, 2024 na itahitimishwa Aprili 19, 2024 Mjini Njombe ambapo atafanya mkutano wa ndani na watendaji mbalimbali wa Chama na kupokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa Mkoa wa Njombe. 


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe