• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Timu ya Wataalamu kutoka Wizara ya Afya yatoa tamko mauaji ya Watoto Njombe.

Tarehe iliyowekwa: February 8th, 2019

Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, imewashukuru waganga wa tiba asili na tiba mbadala kwa ushirikiano katika kuimarisha afya za binaadamu na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Akizungumza na Waganga wa tiba asili na tiba mbadala katika  ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Mwenyekiti wa Timu ya Wataalamu kutoka  Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na  Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Hanifa Selengu amesemu kuwa lengo kuu la wao kufika Mkoani Njombe ni kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa ili kuweza kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea Mkoani Njombe.

“Lengo la safari yetu ni kuja kuungana na kushiriki na Wataalamu wa Mkoa wa Njombe kwa ajili ya kuona namna ya kuzuia au kuondokana na matatizo haya yanayojitokeza ya ukatili na mauaji kwa watoto.Wizara imetoa tamko kwa waganga wote wa jadi  kushirikiana katika kuwafichua waganga wenye kutoa masharti mabaya kwa wanaowahudumia kama wakatafute damu na viungo vya binadamu.”alisema Hanifa

Aidha Wizara imeiomba jamii kuzitumia mamlaka za serikali za Mitaa na jeshi la polisi ili kufichua vitendo vyote viovu vinavyoleta mifarakano miongoni mwao ili hatua stahiki zichukuliwe kwa wakati.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi. Ruth Msafiri amewataka Waganga wa tiba Mbadala na tiba asili katika Halmashauri ya Mji Njombe na wengine Mkoani humo kufanya kazi kwa kufuata utaratibu waliopewa na kuagiza kuondolewa kwa mabango yote mabango yanayotangaza tiba pasipokuwa na kibali maalumu.

“Kama wewe unataka kujitangaza tunakuruhusu lakini fuata taratibu zote za kuhakikisha kuwa tangazo lako linaifikia jamii ulioilenga.Hii ni kwa sababu vibao vingine vyenye matangazo ni vya uchonganishi na mimi sipo tayari kulirihu hili katika wilaya zangu”Alisema Mkuu huyo wa Wilaya.

Akizungumza kwa niaba ya Waganga wa tiba asili Katika Halmashauri ya Mji Njombe Dkt. Mpapai ameishukuru serikali kwa kuwatambua na  kuendelea kushirikiana na wataalamu  hao,na kuomba elimu zaidi iendelee kutolewa kwao ili kuweza kukumbushana majukumu yao na nidhamu katika kazi.

“Tunahitaji elimu ya kutosha mara kwa mara.Tunapata shida kwa kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya majukumu yetu na unakuta tunaweka maslahi mbele.Hakika haya matukio yametuumiza kweli kweli mpaka  tumeanza kuishi kwa hofu na familia zetu.”Alisema Dkt. Mpapai.

Kwa upande wake Mwanasheria kutoka Wizara ya afya,  Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto (Idara kuu ya maendeleo ya Jamii Bw. Denis Bashaka amesisitiza  jamii kufichua vyanzo vinavyosababisha kutokea kwa mauaji hayo na kuangalia namna bora ya kuzifikia jamii kwa kutoa elimu na kuzingatia Sheria, Sera na Miongozo ili kutokomeza vitendo hivyo.

Sambamba na hilo timu hiyo ya Wataalamu kutoka Wizarani ilikutana na  kutoa mafunzo kwa kamati zinazojihusisha na ulinzi na usalama wa mtoto katika Halmashauri ya Mji Njombe,Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  na kuwakumbusha wajibu wao katika kuhakikisha usalama wa mtoto na ilifanikiwa kuandaa jumbe maalumu kwa jamii zitakazorushwa kupitia radio za kijamii  zikilenga kutoa elimu na kusimamia ulinzi na usalama wa mtoto.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe