Wakulima mkoani Njombe wametakiwa kutumia vizuri fursa ya maonesho ya SIDO kitaifa yanayoendelea ili kupata teknolojia itakayowawesha kuanzisha viwanda vya kuongeza thamani mazao yao kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.
Rai hiyo imetolewa Oktoba 23,2023 na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mheshimiwa Exaud Kigahe,wakati wa akifungua maonesho ya nne ya viwanda vidogo SIDO yanayofanyika katika viwanja vya sabasaba mjini Njombe.
Mhe. Kigahe amesema serikali imewekeza kwa kiwango kikubwa kwenye sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi hivyo ili kuunga mkono jitihada za serikali ni lazima teknolojia iendane sambamba na matarajio ya uwekezaji katika sekta ya kilimo ili kupata soko la uhakika.
Amesema kuwa muunganiko wa kilimo na viwanda utakuza soko la ndani na nje ya nchi huku akitoa msisitizo kwa Wakulima kuanzisha viwanda Vidogo.
"Kilimo kiendane na kasi ya uongezaji wa thamani ili kudhibiti upotevu wa mazao, tuunganishe kilimo na viwanda itasaidia kupunguza uagizaji wa bidhaa nje na kuweza kuuza bidhaa zetu nje ya nchi badala yakuuza malighafi" Alisema Mhe. Kigahe.
Aidha amelitaka Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo SIDO kushirikiana na Halmashauri na kuhakikisha vijana wanapata teknolojia ili kuweza kifanya kilimo kibiashara.
Katika hatua nyingine ametoa wito kwa wakulima na wajasarimali mkoani Njombe kutumia fursa yakuzungukwa na nchi mbalimbali kutafuta masoko.
"Njombe ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya chakula, tumie nchi jirani zinazowazunguka kama fursa yakujipatia masoko,serikalini itaendelea kufungua mipaka ili kuongeza masoko sambamba na kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi ili kuongeza uzalishaji pamoja na pato la taifa na mtu mmoja mmoja".
Maonesho ya nne ya Shirika la Kuhudumia Viwanda vidogo SIDO yalianza Oktoba 21 na yamefunguliwa rasmi Oktoba 23,2023 na Mheshimiwa Naibu waziri wa Viwanda na Biashara Exaud Kigahe na yanatarajia kuhitimishwa Oktoba 31,2023.
Maonesho hayo yamebeba kauli mbiu inayosema "Pamoja tujenge Viwanda kwa uchumi na ajira endelevu" yanashirikisha wajasarimali zaidi 800 kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe