• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Usafi wa Mazingira ni Jukumu la Kila Mtu

Tarehe iliyowekwa: September 21st, 2019

Hayo yalisemwa wakati wa zoezi la usafi wa mazingira  lililofanyika katika Mtaa wa Mgendera Halmashauri ya Mji Njombe ikiwa ni maadhimisho ya  siku ya usafi duniani ambayo huadhimishwa kila tarehe 21 Septemba ambapo Wananchi wa Mtaa huo kwa Kushirikiana na wadau wa mazingira  na Wataalamu walishiriki katika kufanya usafi katika eneo ambapo awali lilikuwa linatumika kama eneo la kutupia taka (Dampo).

Akizungumza na Wananchi mara baada ya kukamilika kwa zoezi la Usafi Afisa Mazingira  wa Halmashauri ya Mji Njombe  Nelson Mlwisa alisema kuwa  Wananchi wengi wamejitokeza kufanya usafi jambo ambalo linaonyesha wazi ni kwa jinsi gani uchafu umekuwa kero kwa jamii na jamii imekuwa ikielimika na kustaarabika  kila siku.

“Watu wengi wamejitokeza kufanya usafi katika eneo hili ambalo awali lilikuwa dampo. Mkakati wetu kama Halmashauri ni kuhakikisha kuwa tunaimarisha usafi katika eneo hili muda wote kwa kuzuia watu kutoendelea kutupa taka. Yupo mdau ambaye amejitokeza kwa ajili ya kuliendeleza eneo hili kwa kupanda bustani za maua” Alisema Nelson.

Joseph Mtegea ambaye ni mdau wa mazingira kutoka shirika la SHIPO amesema kuwa licha ya kushiriki mara kwa mara katika kufanikisha shughuli za usafi lakini kama wadau kupitia kitengo cha SMART wamekuwa wakitoa elimu ya mara kwa mara juu ya utunzaji bora wa mazingira kwa kutumia teknolojia na mbinu bora za Kilimo zisizo na athari kwa Mazingira.

Eda Kindole, Rosemeria Sanga Ni wakazi wa Mtaa wa Mgendera ambao wao wamepongeza zoezi la usafi lililofanyika katika eneo la lilipokuwa dampo la zamani katika Mtaa huo kwani wamesema kuwa eneo hilo lilikuwa hatarishi kutokana na aina ya taka zilizokuwa zinatupwa katika eneo hilo.

Jumla ya Wananchi 206 waliweza kushiriki katika zoezi la usafi huku mifuko 540 sawa na Kilogramu 3141 za takataka zikiwa zimekusanywa na kupelekwa eneo la dampo kuu lililopo Maheve, Huku wadau wa mazingira wakiwemo shirika la Nipe fagio, wakishiriki kwa kutoa vifaa kwa ajili ya kufanya usafi.
















Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe