• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Vikundi vilivyopatiwa mikopo vyatakiwa kuzitumia kwa miradi iliyokusudiwa

Tarehe iliyowekwa: February 5th, 2025

Viongozi mbalimbali wamesisitiza umuhimu wa vikundi vilivyopatiwa mikopo kutumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa. Haya yamejitokeza katika hafla ya utoaji wa mikopo kwa vikundi katika Halmashauri ya Mji wa Njombe, ambapo jumla ya shilingi bilioni 1.8 zimetolewa kwa vikundi 111 vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Njombe, Bi. Agatha Mhaiki, alieleza kuwa vikundi hivyo vilikidhi vigezo vyote vya kupatiwa mikopo, hivyo ni jukumu lao kuhakikisha fedha zinatumika kwa miradi iliyokusudiwa.


"Tumekopa, tulileta maandiko yenye tija. Naomba fedha tulizopata tuzitumie kama tulivyokusudia," alisisitiza Bi. Agatha.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Bw. Samson Medda, aliwasihi wanufaika kuwa waadilifu na kuhakikisha mikopo wanayopata haitumiki kwa matumizi yasiyo na tija. Pia aliwakumbusha kurejesha mikopo kwa wakati ili kutoa fursa kwa wengine kunufaika.


"Mkaitendee haki mikopo hii, fanyeni kazi kwa bidii, zingatieni malengo ya vikundi vyenu. Mikopo hii siyo sadaka, inapaswa kurejeshwa ili wengine nao waweze kufaidika," alisema Bw. Medda.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Nestory Mahenge, alibainisha kuwa vijana mara nyingi wamekuwa kundi linaloshindwa kurejesha mikopo kwa wakati, akiwataka kubadilika ili kufungua fursa zaidi kwa wenzao.


"Mikopo hii tuitumie kama tulivyopanga. Vijana, fedha hizi ni fursa kwa wenye malengo na nidhamu, natamani kuona tukipiga hatua kuelekea kwenye viwanda kupitia mikopo hii," alisema Mhe. Mahenge.

Naye Diwani wa Viti Maalum, Mhe. Angela Mwangeni, aliwataka wanawake waliopokea mikopo kuendelea kuwa mfano mzuri kwa kurejesha kwa wakati.


"Fedha imetolewa kwa wingi kwa wanawake, msiniangushe. Mmeonyesha uaminifu kwa kurejesha vizuri, tuendelee kushirikiana mpaka tumalize marejesho. Vijana, naomba msisite kurejesha mikopo," alisisitiza.

Wanufaika wa mikopo hiyo pia walipata fursa ya kupata elimu ya rushwa kutoka TAKUKURU pamoja na ufafanuzi wa sheria na kanuni za mikopo  na adhabu zinazoweza kutolewa endapo vikundi vitashindwa kufanya marejesho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe