Wazazi na walezi katika kijiji cha Luponde wamehimizwa kubadilika kwa kuhakikisha watoto wao wanapatiwa vyakula vinavyotokana na kundi la wanyama kama vile nyama,maziwa,mayai ,wadudu(senene kumbikumbi),jibini mazao ya baharini kama vile samaki na dagaa ili kuondokana na hali duni ya lishe inayosababisha udumavu kwa watoto.
Akizungumza na wananchi waliohudhuria kwenye Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji (SALIKI) iliyofanyika Mei 28,2024 kijijini hapo Afisa usimamizi wa shughuli za lishe wa USAID Lishe Project Jeris Muhiny,amesema kundi hilo lenye virutubisho aina ya protini pamoja na umuhimu wake wa kujenga mwili wakati wa ukuaji wa mtoto halizingatiwi na familia nyingi Mkoani Njombe.
Ameeleza kuwa watoto wengi hupatiwa makundi ya vyakula yasiyozidi matatu na kati yake hakuna nyama,samaki au mayai jambo ambalo linachangia watoto kuwa na uzito pungufu na wengine kupata utapiamlo na udumavu ambao ni changamoto kubwa kwa mkoa wa Njombe.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe