• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Vyoo aina ya "SATO" vyaanza kutumika Njombe.Mafundi wajengewa uwezo

Tarehe iliyowekwa: June 9th, 2021

Halmashauri ya Mji Njombe kwa kushirikiana na Kampuni ya Lixil ambayo ni  watengenezaji wa vyoo aina ya “SATO” imetoa mafunzo kwa mafundi sitini katika kila Kijiji na Mtaa,katika Halmashauri hiyo  ili kutimiza lengo la kuhakikisha kuwa kila Taasisi na Kaya inakuwa na  vyoo bora na salama.

Akizungumzia lengo la mradi wa uboreshaji vyoo Meneja wa Kampuni ya Lixil Justine Mbowe amesema kuwa wazo hilo lililotokana na jitihada za kuboresha mazingira katika ngazi ya Kaya na Taasisi ambapo kwa mwaka 2018 Kampuni hiyo ilitoa idadi ya vyoo elfu themanini  kwa Serikali kupitia wizara ya Afya kupitia kampeni mbalimbali za usafi ikiwemo kampeni ya nyumba ni choo ili Wananchi wenye uhitaji na wa hali ya chini waweze kupata fursa ya kuboresha vyoo vyao na kuwa na mazingira salama.

“Licha ya kuwapatia elimu mafundi tumeona pia tutoe elimu hii katika Shule za Msingi kwani tunaamini tabia huanza kujengwa toka mtoto anapokuwa mdogo. Hii inamaana kuwa watoto watakapopata elimu hii ya matumizi ya vyoo hivi kuanzia shuleni watakuwa ni mabalozi wazuri katika kaya zao. Kwa upande wa wanafunzi wa Shule za Msingi tunaamini ni rahisi kwao kuendeleza matumizi ya choo bora tangu  wakiwa na umri mdogo.”Alisema Mbowe

Kwa upande wake Afisa Afya Halmashauri ya Mji Njombe Saimon Ngassa amesema kuwa madhumuni ya ujenzi wa vyoo kwa kutumia masinki ya plastiki aina ya “SATO” ni muendelezo wa Kampeni mbalimbali za uboreshaji wa Mazingira na kwa sasa Halmashauri inaendelea na Kampeni ya uboreshaji wa vyoo katika maeneo ya Taasisi na Kaya ambapo kwa sasa kampeni hiyo imelenga kuboresha vyoo vya asili kwa kuviwekea masinki ya vyoo vya plastiki na yanayoendana na mazingira halisi.

“Tumejifunza kuwa vyoo hivi vinatumia maji kidogo na ufanisi wake ni mkubwa katika kuzuia harufu na wadudu wanaoingia kwenye vyoo na kwenda kwenye makazi jambo litakaloweza kupunguza maradhi kwa kiasi kikubwa lakini pia ni vyoo vyenye gharama nafuu kwa Wananchi wenye kipato cha chini.”Alisema Ngassa.

Aliendelea kusema “Kampeni hiyo inatekelezwa kwa kuwajengea uwezo mafundi wa eneo husika ambapo kila Kijiji kilitoa fundi mmoja kwa ajili ya kupatiwa mafunzo ili wawewatekelezaji katika kuboresha na kuwajengea vyoo bora Wananchi ngazi ya kaya.”

Johnson Joseph, Bisaya Musa Wanafunzi kutoka shule ya Msingi Kisilo kwa pamoja wanasema kuwa changamoto iliyokuwepo katika vyoo vya mashimo ni uwepo wa harufu kali na wadudu kutoka chooni kusambaa jambo ambalo limepatiwa ufumbuzi kupitia vyoo vipya na wamesema kuwa vyoo hivyo vitasaidia kwenye uthibiti wa magonjwa mbalimbali na atawashauri wazazi kuwa na vyoo hivyo

Patrick Mdetele Fundi kutoka Kijiji cha Utalingolo na Kutoka Rocks Mwalongo kutoka  Kijiji cha Idihani wamesema kuwa elimu hiyo inamanufaa makubwa kwao hususani kwa Wananchi watakaowahudumia kwani gharama ni nafuu ukilinganisha na masinki ya aina nyingine na uwepo wa mfuniko ni mdhibiti tosha wa uchafuzi wa mazingira kwa njia ya hewa.

Mkoa wa Njombe umepatiwa jumla ya vyoo 1630  ambapo mpaka sasa Shule za Msingi 33 kutoka Halmashauri ya Mji Njombe zimeweza kujengewa vyoo vya masinki ya “SATO” huku Wananchi wakihamasishwa kutumia teknolojia hiyo na kwa wenye uhitaji waweze kuwasiliana na maafisa afya na watendaji wa vijiji,mitaa na Kata husika ili kuweza kufungiwa vyoo hivyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe