• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WADAU WA MAENDELEO WAOMBWA KUCHANGIA UJENZI WA SHULE SHIKIZI KAMBARAGE

Tarehe iliyowekwa: October 10th, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe Erasto Mpete amewaomba Wadau wa Maendeleo, Wananchi na Taasisi mbalimbali kuchangia ujenzi wa Shule shikizi ili kuwapunguzia adha wananchi na Wanafunzi wanaoishi eneo la Block (X) lililopo kata ya Njombe Mjini.


Mhe Mpete ametoa rai hiyo Oktoba 10,2023 alipotembelea eneo hilo la Block (X) ambalo litajengwa Shule Shikizi itakayokuwa na vyumba vya Madarasa vitatu (3) Ofisi moja (1) na Matundu ya vyoo Nane (8).


Mhe Mpete amesema ametembelea Eneo hilo kutokana na mwamko mkubwa wa wananchi wa mtaa huo kuhitaji kutatua changamoto iliyopo kwenye eneo lao ambapo kwa jitihada za wananchi Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe imetoa kibali cha ujenzi wa Shule shikizi katika eneo hilo.


" Niwaombe wananchi,Taasisi mbalimbali na wadau wa Maendeleo kuweza kuchangia Ujenzi wa Shule hii ili kwa pamoja tuweze kupunguza changamoto kwa watoto wetu wanaotembea umbali mrefu,Hivyo tunaomba watu wetu walioteuliwa kuchangisha mchango wa Ujenzi wakipita kuomba mchango wa kuchangia ujenzi huu tusisite kutoa,na ambaye anaweza kutoa chochote tunaomba atusaidie kama vile Mchanga au mawe ili Tukamilishe kwa wakati"Alisema Mhe Mpete.


Kwa Upande wake Amosi Luhamba Afisa Mipango miji wa Halmashauri ya Mji Njombe amesema Eneo hilo lina ukubwa wa Ekari 1.8 na ujenzi wa Kituo hicho utawasaidia wananchi wa mtaa huo kutatua changamoto na kuwalinda watoto wao huku akitoa ombi kwa wananchi wa mtaa huo kuhakikisha wanatunza mazingira kwa Kupanda Miti ambayo itasaidia kuongeza hewa safi.


Kwa upande wake Mtendaji wa Kata ya Njombe mjini Enos Lupimo amesema wamejipanga kuhakikisha ujenzi wa shule hikizi unaenda kwa kasi kubwa huku akisisitiza wananchi kuunga mkono ujenzi huo.


Ujenzi wa Shule Shikizi ya mtaa wa Block (X) utapunguza changamoto ya wanafunzi wa eneo hilo kuacha kutembea umbali mrefu na kuacha kupita kwenye maeneo hatarishi ikiwemo barabara kuu ya Songea wakati wa kwenda shule Jirani za Mji mwema,Nazarèth na Sabasaba.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe