Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi. Kuruthum Sadick, Februari 15,2024 alipokea matunda ya parachichi yaliyotolewa na kampuni ya AVO GROUP kwa ajili ya kuwapitia wanafunzi na watoto wanaohudhuria kliniki kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.
Zoezi la ugawaji wa matunda hayo lilifanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe likiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Anthony Mtaka.
Lengo la kutoa matunda hayo ni kuunga mkono juhudi za Serikali Mkoani Njombe kupambana na Udumavu.
Mkoa wa Njombe unaendesha kampeni yenye mpango mkakati wa miaka 7 ili kupunguza udumavu ambao unatajwa kuwa ni asilimia 50.
Kampeni hii ya Lishe ya mwanao Mafanikio yake yenye Kaulimbiu mbiu "Kujaza tumbo siyo lishe, Jali unachomlisha", inalenga kutoa elimu ya lishe bora kwa mama mjamzito na watoto wenye umri chini ya miaka 5 pamoja na vijana rika balehe, ili kuwa andaa kuwa baba na mama bora.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe