• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WANANCHI NJOMBE WASHAURIWA KUZINGATIA MPANGO KABAMBE UENDELEZAJI MJI

Tarehe iliyowekwa: July 22nd, 2022

Ni katika Mkutano wa mwaka wa baraza la Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Mji Njombe ambapo, Mbunge wa jimbo la Njombe Mjini Mheshimiwa Deo Mwanyika amewataka Wananchi waliopo katikati ya Mji Njombe kuhakikisha kuwa wanazingatia mpango kabambe wa Halmashauri kwenye ujenzi wa nyumba ili kuifanya Halmashauri ya Mji Njombe kukidhi vigezo vya kuwa Manispaa.

Mwanyika amesema kuwa licha ya kuwa kumekuwa na maboresho ya ujenzi katika maeneo mengi hususani katikati ya Mji, lakini bado Wananchi wengi wamekuwa hawazingatii mpango kabambe wa Mji  kwani ujenzi ambao umekua ukiendelea kufanyika ni ujenzi wa nyumba za kawaida na sio ujenzi wa maghorofa kama ilivyoainishwa katika mpango huo wa ujenzi katikati ya Mji.

“Bado kwenye maeneo yetu ya Mji Ujenzi unaofanyika sio wa magorofa, ujenzi unaofanyika ni wa kizamani jambo ambalo litaweza kutuchelewesha kupata Manispaa.”Alisema Mheshimiwa Mbunge.

Akizungumza katika mkutano wa Baraza la Mwaka la Waheshimiwa Madiwani Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mheshimiwa Erasto Mpete amewapongeza Wataalamu, na Waheshimiwa Madiwani kwa kuiwezesha Halmashauri katika mwaka wa fedha 2021-2022 kukusanya kwa asilimia 141.9 za makusanyo ya ndani jambo ambalo litaiwezesha Halmashauri kutekeleza miradi mingi ya maendeleo.

Wakitoa maoni yako katika mkutano huo baadhi ya Waheshimiwa Madiwani Edwin Mwanzinga Diwani wa Kata ya Matola amesema kuwa licha ya kuwa jitihada kubwa zimefanyika za ukusanyaji mapato lakini bado usimamizi madhubutu unahitajika katika matumizi ya fedha zinazokusanywa ili kuweka nidhamu  ya fedha hizo lakini pia kuepuka upanuzi wa vifungu kutokana na bajeti zilizokuwa zimepangwa kushindwa kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Naye Diwani wa Kata ya Ramadhan Nickson Nganyange amesema bajeti ya mwaka 2021/2022 imekua ni ya mafanikio makubwa kwani imeweza kufanikisha utekelezaji wa miradi mingi ya maendeleo jambo ambalo limeiletea heshima Halmashauri

Michael Uhaula  Diwani wa Kata ya Yakobi amesema kuwa mafanikio yaliyofikiwa katika Kata yake ni pamoja na kufanikisha kuanza kwa kidato cha tano katika shule ya Sekondario Yakobi na pia amewashukuru  Wananchi wa Yakobi kwa kuendelea kuchangia kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Awali Baraza hilo lilitanguliwa na uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ambapo Mheshimiwa Filoteus Mligo Diwani wa Kata ya Lugenge alichaguliwa kwa kura za ndio 14 kati ya kura 14 zilizopigwa na hivyo kuidhinishwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri kwa kipindi cha mwaka 2022-20223. Aidha Baraza hilo lilifanikiwa kufanya uchaguzi wa Wenyeviti na kuunda kamati za kudumu za Halmashauri, Bodi ya Ajira na ALAT pamoja na kupitia na kuidhinisha ratiba ya vikao mbalimbali vya Kisheria.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe