• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Wananchi tushirikiane kukamilisha miradi ya UVIKO kwa wakati

Tarehe iliyowekwa: December 3rd, 2021

Rai hiyo imetolewa wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa Wilaya ya Njombe yenye lengo la kuangazia utekelezaji wa Ilani ya CCM ambapo walitembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Kata tatu za Njombe Mjini, Mjimwema na Ramadhani ujenzi unaotekelezwa kupitia fedha za mapambano dhidi ya Uviko, na ambao kutokana na maelekezo ya Serikali ujenzi huo unatakiwa kukamilika kufikia desemba 15 mwaka huu.

  Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati Edward Mgaya amesema kuwa kwa kipindi kilichosalia ni vyema nguvu kubwa ya ujenzi iongezwe ili miradi hiyo iweze kukamilika kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali na amewataka Wenyeviti wa Mitaa na Watendaji  kuhakikisha kuwa wanawahamasisha Wananchi kwa kupangiana zamu  kushiriki kwenye kusaidia shughuli za ujenzi ili kuongeza nguvu kazi na kasi kwenye miradi hiyo.

“Muda uliobaki si rafiki, katika maeneo mengine ya Wilaya ya Njombe tumeona ushiriki mkubwa wa Wananchi katika eneo la ujenzi kuhakikisha kuwa miradi hii inakamilika. Katika Kata hizi za Mjini naona kunachangamoto ya ushiriki wa Wananchi. Tukiwategemea mafundi pekee hatuwezi kukamilisha hili kwa wakati. Wananchi wanapaswa kufahamu kuwa wanawajibika katika kusaidia kwani fedha hizi za ujenzi zisingeletwa na Serikali Wananchi wangepaswa kuchanga kujenga madarasa. Sasa tumeletewa fedha za ujenzi kwanini wasisaidie? Miradi tunataka ikamilike kufikia tarehe 15 na kwa ubora hivyo wekeni mikakati mizuri ya kufanikisha hili.”Alisema Mgaya

Katika hatua nyingine wajumbe wa kamati hiyo wamelaani vikali tukio lililofanywa na Wananchi wasio wema kwenye Kata ya Mjimwema kwa kuvunja masinki ya vyoo 11katika Shule mpya ya Mjimwema jambo lilaloitia hasara Serikali lakini pia kuwaongezea mzigo Wananchi kuchangia tena kununua masinki mapya ili kurejesha katika vyoo vyote ambavyo masinki yake yaliharibiwa.

Kwa upande wake katibu wa CCM Wilaya ya Njombe Sure Mwasanguti amepongeza kasi ya ujenzi katika Shule ya Sekondari Mpechi ambayo kwa sasa ipo katika hatua ya upigaji wa lipu na ameupongeza Mtaa wa Kambarage kwa kujitoa kuchangia ujenzi wa Shule mpya ya msingi Kambarage B ambapo kwa kiasi kikubwa shule hiyo itasaidia kupunguza msongamano wa Wanafunzi katika shule ya  Kambarage.

“Kwenye fedha tulizopewa na Serikali tunahitaji kila kitu kikimbie. tunapokimbiza maendeleo yanaisha vizuri ila tunapochelewesha tunabaki palepale. Mji wetu hauwezi kukuwa kama tusiposhirikiana kwa pamoja” Alisema Mwasanguti.

Licha ya Kamati kukagua miradi 3 ya vyumba vya madarasa vyenye thamani ya shilingi milioni 360 ikiwa ni fedha za mapambano ya UVIKO,ukaguzi mwingine ni ujenzi wa Shule mbili mpya za msingi ujenzi unaofanywa na nguvu za Wananchi,wadau na Halmashauri na ujenzi wa kituo kipya cha Afya Mjimwema ambacho kitasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika kituo cha Afya Njombe Mjini.Pia  Kamati hiyo  pia imekagua shughuli za Kilimo cha miche ya parachichi kinachofanywa na moja ya kikundi cha Wanawake Mjimwema kikundi kilichopatiwa milioni 10 kutoka kwenye asilimia kumi ya mikopo ya Wanawake,Vijana na Walemavu na kufurahishwa na shughuli yao kwani thamani ya fedha na mradi unaoendelea vinatija iliyokusudiwa.

Aidha.Kamati hiyo imekagua ujenzi wa Daraja linalounganisha Kata ya Ramadhani na Njombe Mjini na ujenzi wa Barabara ya lami katika Mtaa wa Idundilanga ujenzi unaotekelezwa na Wakala wa barabara Vijijini na Mjini Wilaya ya Njombe (TARURA) .

Halmashauri ya Mji Njombe imepokea kiasi cha Shilingi milioni 740 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 37 katika shule 12 za Sekondari na shilingi milioni 80 ikiwa ni ujenzi wa bweni la Wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Shule ya Msingi Kibena na hivyo kufanya jumla kuu ya fedha zilizopokelewa kuwa shilingi milioni 820 hii ikiwa ni fedha za mapambano ya UVIKO 19.

                                                                                   

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe