• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WANANCHI WASHUKURU ,UJENZI WA KITUO CHA AFYA.

Tarehe iliyowekwa: September 11th, 2024

Wananchi wa Kata ya Kifanya, Halmashauri ya Mji Njombe, wameishukuru Serikali kwa kuwajengea kituo cha afya chenye miundombinu na vifaa vya kisasa, ambacho kitawasaidia kuondokana na tatizo la kutembea umbali wa kilomita 50 kwenda hospitali ya Kibena Mjini Njombe kwa ajili ya huduma za afya. 


Wakizungumza Septemba 11, 2024 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), iliyotembelea kituo cha afya cha Muungano kilichopo Kata ya Kifanya, wananchi hao walieleza kuwa awali walilazimika kusafiri umbali mrefu kupata huduma za afya, lakini sasa hali imebadilika kwa sababu wanapata huduma hizo karibu. 


"Tulilazimika kusafiri hadi hospitali ya Kibena au Ikonda iliyopo wilaya ya Makete, ambako ni mbali sana. Tunaishukuru sana Serikali kwa kuboresha huduma za afya na kujenga majengo mapya," alisema Romanus Tweve, mmoja wa wananchi. 


Diwani wa Kata ya Kifanya, Mheshimiwa Nolasco Mtewele, alieleza kuwa ujenzi wa kituo hicho ulianzishwa na wananchi wenyewe, na baadaye Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ilileta fedha zaidi ya milioni 500 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo. 


"Naomba mtufikishie salamu zetu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha na vifaa tiba kwa ajili ya kituo hiki," Alisema Mhe.Mtewele. 


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI, Justine Nyamoga, aliipongeza Serikali kwa kuendelea kuboresha huduma za afya mijini na vijijini. 


"Sisi kama Bunge tumeridhishwa sana na utekelezaji wa miradi tunayokutana nayo. Kituo hiki cha afya Muungano Kifanya ni mfano wa uboreshaji wa huduma za afya katika maeneo ya vijijini. Tumeona chumba cha upasuaji ambacho kinaendana na viwango vya kisasa sawa na vile vilivyopo katika hospitali kubwa," Alisema Mhe.Nyamoga. 


Jumla ya muondombinu mipya sita (6) imejengwa katika kituo cha afya Muungano Kifanya ambayo ni, Jengo la mama na mtoto,Mionzi,maabara,jengo la kufulia, jengo lakuhifadhia maiti,jengo la upasuaji  pamoja na Njia (walkways).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe