• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Wanufaika TASAF Njombe wahamasishwa kuweka akiba

Tarehe iliyowekwa: June 21st, 2019

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Nchini TASAF kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini TASAF III Umetoa elimu kwa vikundi 14 vya Wanufaika wa Mpango huo kuhusu uwekaji akiba na kukuzaji uchumi katika Kata za Utalingolo na Uwemba zilizopo katika Halmashauri ya Mji Njombe.

Akizungumza malengo ya elimu ya vikundi kwa wanufaika wa TASAF Afisa Ufuatiliaji Kitengo cha Maendeleo ya Miundombinu TASAF Ndg. Augustino Ngude amesema kuwa lengo kuu la mpango huo ni kukuza utamaduni wa kujiwekea akiba kwa kaya maskini ili kuwawezesha kukabiliana na dharura na mahitaji ya msingi pasipo kutegemea ruzuku ya TASAF.

“Tunatoa elimu hii ya uundwaji wa vikundi na kuweka akiba kwa wanufaika wa Mpango wa kunusuru kaya maskini ili kufanya mradi uwe endelevu. Kila mradi huwa na mwanzo na mwisho ila tunategemea kupitia vikundi ambavyo wameshavianzisha vitawasaidia wanufaika hao hata pale ambapo mradi utakapokuwa umefikia ukomo.”Alisema

Ngude aliendelea kusema “Vikundi 14 tulivyovitembelea kwa siku mbili hizi vimekuwa vikifanya vizuri kwenye kuweka akiba. Yapo maeneo ambayo walikuwa wanakwama kutokana na ukosefu wa elimu ya akiba na utunzaji kumbukumbu za fedha kwenye kikundi .Mafunzo tuliowapatia yamewasaidi kubaini wapi walikuwa wanakosea na namna bora ya kuboresha kile walichoanzisha. Naomba nitoe rai kwa wawezeshaji kuendelea kuvitembelea vikundi hivi mara kwa mara ili kuendelea kutoa elimu zaidi” Alisema

Mark Salema, Henry Kideula, Christina Tsangai na Mariam Monjesa  ni Wawezeshaji TASAF Ngazi ya Halmashauri ambao wao kwa pamoja wamepongeza mwitikio wa wanufaika hao kujiunga katika vikundi vya kuweka akiba na kukuza uchumi na kubaini changamoto kubwa inavyovikabili vikundi hivyo kuwa ni ukosefu wa elimu juu ya  utunzaji wa  kumbukumbu za fedha kwenye kikundi na Wanakikundi kuweka kiwango kikubwa cha akiba ukilinganisha na kipato wanachopata huku muda wa kukutana ukiwa mrefu changamoto inayofanya wanakikundi wengine kushindwa kuendelea na wengine kushindwa kukopa kwa wakati.

Wawezeshaji hao wamesema kuwa kupitia mafunzo hayo wameweza kuwaelekeza wanufaika  kuweka akiba kidogo kulingana na kipata chao huku wakiendelea kujishughulisha kwenye  miradi midogo midogo itakayowaingizia kipato cha kudumu badala ya kutegemea ruzuku  ya TASAF na kuwahamasisha wanakikundi kukutana angalau kila wiki ili kuweza kuwa na taarifa za mara kwa mara za kikundi na pia itasaidia Wanakikundi kukopa na kurejesha kila wakati na kuondokana na kupata faida kidogo wakati wa mgawanyo.

Kwa upande wao Wanufaika wa Mpango huo Bi Foida Samwel kutoka kikundi cha Muungano ambao mpaka sasa kikundi chao kina kiasi cha Shilingi Laki saba na Bi Sixbetha Mpete kutoka kikundi cha Upendo na Kazi ambacho kina zaidi ya Shilingi milioni tatu vyote kutoka Uwemba, wamesema kuwa wanaishukuru TASAF Kwa mafunzo hayo kwani yamezidi kuwapa mwanga wa kuendelea kupambana na umaskini kwa kufanya kazi kwa juhudi  na kuweka akiba ili kuendelea kuboresha maisha.

Mpaka sasa Halmashauri ya Mji Njombe imefanikiwa kuunda vikundi 123 vya wanufaika katika Kata 13 na imeanza kutoa elimu kwa vikundi 14 katika awamu ya kwanza na inaendelea na zoezi la utoaji elimu ya uwekaji akiba kwa vikundi vilivyosalia ili kuvijengea uwezo zaidi. Ikumbukwe kuwa TASAF II ilionyesha mafanikio makubwa katika kuunda vikundi ambapo vikundi 1172 viliundwaa na kati ya hivyo vikundi 1000 vilipatiwa mafunzo na vifaa kwa ajili ya uwekaji wa akiba kwa vikundi  na wanufaika walitumia akiba zao kubadili hali zao za maisha.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe