• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WAZAZI NA WALEZI NJOMBE WAHAMASISHWA MALEZI BORA YA WATOTO.

Tarehe iliyowekwa: August 18th, 2025

Mkufunzi wa sayansi ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ngazi ya Taifa, Martini Chuwa, amewataka wazazi na walezi Mkoa Njombe kuhakikisha watoto wanapata malezi bora, lishe sahihi, na vichezeo (vichangamgamshi) vinavyowasaidia kielimu na kihisia. 


Akizungumza Agosti 18,2025 na wakazi wa Soko Kuu Njombe, Chuwa alisema kuwa malezi bora hayahusishi tu huduma za msingi kama chakula, malazi, afya na usalama, bali pia upendo, mwongozo wa maadili, nidhamu chanya, na msaada wa kihisia unaomjenga mtoto kimaadili na kisaikolojia akiwa katika makuzi.

Akiendelea kuzungumza na wananchi wa Soko kuu Njombe Chuwa alisisitiza umuhimu wa wanaume kushiriki kikamilifu katika malezi ya watoto wao badala ya kuachia jukumu hilo kwa wanawake pekee.  


“Malezi bora lazima yawe ya kisayansi na yenye kuzingatia hatua za ukuaji wa mtoto, wanaume msiwaachie wanawake kwasababu watoto wanahitaji malezi yapande zote mbili ,mtoto wakike atatamani kuishi vizuri na mwanaume kupitia baba yake na mtoto wakike atataka kujifunza kuishi vizuri na mke wake kupitia mama yake anavoishi jambo ambalo litawasaidia wakiwa wakubwa kumjuwa mke bora ni yupi na mwanume bora ni yupi” aliongeza Chuwa. 


Kwa upande wake, Afisa Lishe wa Mkoa wa Njombe, Bi. Bertha Nyigu, kupitia Mradi wa Lishe ya Mwanao unaosimamiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Njombe na kudhaminiwa na UNICEF, aliwataka wazazi hususani wale wanaoshinda sokoni kuhakikisha wanawapeleka watoto wao katika Kituo cha Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Watoto kilichopo Soko Kuu Njombe kwa lengo la kupunguza changamoto ya udumavu miongoni mwa watoto ambayo bado ipo katika mkoani Njombe. 


Ni jukumu la kila mlezi kuhakikisha watoto wanapata malezi bora, lishe yenye afya, na mafunzo ya maadili mema na malezi bora yatakayosaidia mtoto kukua akiwa na nidhamu, upendo, na mwongozo wa maadili, na lishe sahihi itakayomsaidia kupata afya njema na ukuaji wa kisaikolojia jamba ambalo litasaidai kuwaandaa watoto kuwa raia wenye uwezo wa kuchangia maendeleo ya familia, jamii, na taifa kwa ujumla.

#maendeleokwawote 

#maleziyawatoto 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA YASISITIZWA KWA WAKULIMA WA MTAA WA MPOBOTA - MJIMWEMA .

    October 11, 2025
  • MWEKEZAJI MADEBE AKABIDHIWA HATI MILIKI 16

    October 11, 2025
  • WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 11, 2025
  • HERI YA SIKU YA MTOTO WA KIKE.

    October 11, 2025
  • Angalia zote

Video

IFAHAMU HUDUMA YA KIPEKEE INAYOPATIKANA NDANI YA SOKO KUU NJOMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe