• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Wazazi watakiwa kuimarisha ulinzi wa Watoto Msimu wa Sikukuu

Tarehe iliyowekwa: December 17th, 2024

Tarehe 16 Disemba 2024  Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Mji Njombe, Vickiana Kiwelu, ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha wanalinda watoto wao dhidi ya ukatili wa kijinsia wakati wa msimu wa Sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya.


Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Ofisi ya Mtaa wa Lunyanywi, Kiwelu alisisitiza umuhimu wa jamii kuwa mabalozi wa kupinga ukatili dhidi ya watoto. Alihimiza pia wananchi kuheshimu utu na kuepuka kujichukulia sheria mkononi wakati changamoto zinapojitokeza.


"Niwaombe wananchi, katika kipindi hiki cha sikukuu, tuwalinde watoto wetu. Tunapopokea wageni majumbani mwetu, si kila mtu anakuja kwa nia nzuri. Kama nyumba yako ni ndogo na unalazimika kumpa mgeni hifadhi, tafuta mahali pa kumpeleka mbali na watoto ili kuwaepusha na hatari ya ukatili," alisema.


Aliongeza kuwa wazazi wanapaswa kuwa waangalifu, hasa wakati wa msimu wa sikukuu ambapo mara nyingi hutembelewa na ndugu na marafiki. Alikumbusha kuwa baadhi ya watu hujificha nyuma ya uhusiano wa kifamilia huku wakiwa na nia mbaya.


Aidha, alizungumzia changamoto ya wazazi waliotengana kutotimiza wajibu wa kuwalea watoto wao, akibainisha kuwa kumekuwa na ongezeko la akina mama kufika ofisi za serikali kudai matunzo kutoka kwa wenza wao.


"Naomba wazazi wote, hasa wale waliotengana, wahakikishe wanatimiza wajibu wao wa kuwalea watoto. Watoto wanahitaji matunzo na malezi bora, si jukumu la mama peke yake au baba peke yake," aliongeza.


Wito huo umelenga kuhimiza wazazi na jamii kwa ujumla kuchukua hatua za tahadhari ili kuhakikisha watoto wanalindwa na kupatiwa mazingira salama, hasa katika msimu huu wa sikukuu unaohusisha mwingiliano mkubwa wa kijamii.


@ortamisemi @maendeleoyajamii @kissagwakisakasongwa @njombe_rs

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe