• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WAZIRI MKUU MAJALIWA AFUNGUA RASMI MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025.

Tarehe iliyowekwa: June 9th, 2025

Na -  OR-TAMISEMI,  Iringa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amezitaka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kushirikiana kikamilifu katika kukamilisha mradi wa ujenzi wa shule 56 za kuendeleza vipaji vya michezo.


Mhe. Majaliwa ametoa agizo hilo leo, Juni 9, 2025, wakati wa ufunguzi rasmi wa mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi (UMITASHUMTA) na Sekondari (UMISSETA), yaliyofanyika katika Viwanja vya Kichangani, Kata ya Kihesa, Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa.

Aidha, amezitaka Ofisi ya Rais – TAMISEMI pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kuhakikisha kuwa ratiba za michezo zinawekwa rasmi kwenye mipango ya kila shule na kutekelezwa ipasavyo ili kutoa nafasi kwa wanafunzi kushiriki michezo mara kwa mara kwa lengo la kukuza vipaji.


> "Katika shule zetu tunahitaji ratiba za michezo ili vijana wetu baada ya masomo waweze kushiriki katika shughuli za michezo. Hili litasaidia kuinua vipaji na kuwaandaa kwa mashindano haya ya kitaifa," alisema Waziri Mkuu.


Mhe. Majaliwa amevitaka vyama vya michezo vya kitaifa kupeleka wataalamu kwenye mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA ili kuwabaini wachezaji wenye vipaji maalum watakaoendelezwa kwa lengo la kuunda timu bora za taifa.

Aidha, amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote kuhakikisha walimu wa michezo wanapewa mafunzo maalum ya kisasa kuhusu sheria, mbinu na mabadiliko ya michezo, na kuwapeleka kwenye vyuo vya michezo vilivyopo nchini ili kuongeza ufanisi wa ufundishaji.


Waziri Mkuu pia ameagiza Kituo cha Mafunzo cha Malia kutumika kikamilifu kwa ajili ya kuwajengea uwezo walimu wa michezo ili kusaidia kukuza vipaji vya wanafunzi katika ngazi ya shule.


Vilevile, amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha maeneo ya wazi yaliyotengwa kwa michezo hayavamiwi na shule zote za msingi na sekondari zinakuwa na viwanja kwa ajili ya michezo mbalimbali inayoshirikishwa kwenye mashindano haya.


Ameitaka TAMISEMI, kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kuandaa mpango mkakati wa kitaifa utakaohakikisha kila shule inakuwa na miundombinu ya michezo, ikiwemo viwanja vya riadha, ili kuimarisha ushiriki wa wanafunzi katika michezo.


Pia, amezihimiza taasisi hizo kushirikiana na wadau wa michezo, kama makampuni ya biashara yanayodhamini michezo, kuendeleza vipaji vilivyoibuliwa mashuleni kwa lengo la kuzalisha wanamichezo bora.


Kwa upande mwingine, Waziri Mkuu ameitaka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoa vibali kwa shule binafsi na academies zinazolenga kukuza vipaji vya michezo kuanzia ngazi ya awali, ili ifikapo umri wa miaka 14 vijana wawe wameimarika kitaaluma na kimwili.


Mwisho, amewataka Watanzania wote kujenga tabia ya kufanya mazoezi ya viungo mara kwa mara ili kuwa  na afya bora ambayo ndio msingi wa taifa lenye nguvu.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe