• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

"Wilaya ya Njombe imeupiga mwingi utekelezaji wa miradi."Kamati ya Siasa wa Njombe yakiri

Tarehe iliyowekwa: December 10th, 2021

Ni katika ziara ya siku moja yenye lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM, ambapo Katibu wa Siasa na uenezi Mkoa wa Njombe Erasto Ngole amesema kuwa Wilaya ya Njombe imeweza kuendelea kutekeleza miradi mizuri yenye ubora na itakayolenga kutatua kero kwa Wananchi.

Akizungumza mara baada ya kukagua miradi inayotekelezwa kwa fedha za mapambano ya Uviko na miradi inayojengwa kupitia nguvu za wananchi na Mapato ya ndani ya Halmashauri kikiwemo Kituo cha Afya Mjimwema na Ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa shule ya sekonari mpechi Ngole amesema kuwa Serikali imeendelea kufanya kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa maendeleo ya wanawafikia wananchi.

“Niwapongeze Wananchi wa Kata ya Mjimwema kwa kuamua kuanza ujenzi wa kituo cha afya. Kituo hiki kitasaidia kutatua changamoto ya kituo kilichopo eneo la mjini ambacho kinahudumia Wananchi wengi. Kata ya Mjimwema ni Kata ya kimkakati ndipo yalipo Makao makuu ya mkoa na ndipo eneo ambalo mji unapokua.Kkituo hiki kitakua na msaada mkubwa kwani Taasisi nyingi za Kiserikali zitakapokuwa. Niombe Mkurugenzi kuhakikisha kuwa unatoa kipaumbele kupitia mapato ya Halmashauri kuhakikisha kuwa ujenzi wa Kituo hiki unaendelea ili uweze kukamilika na wananchi kupata huduma.

Katika Shule ya Sekondari Mpechi shule iliyonufaika na ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa vyenye thamani ya shilingi milioni 100 mradi  unaotekelezwa kupitia fedha za mapambano ya UVIKO mwenezi wa Mkoa wa Njombe amesema kuwa anashangazwa na baadhi ya Wananchi wanaopinga jitihada za Rais katika kuletea maendeleao kwa kuboresha mahusiaono na Mataifa mbalimbali na amesema kuwa tabia hiyo inapaswa kukemewa vikali
“Ndugu zangu katika kipindi kama hiki miaka iliyopita wazazi walikua hawakai majumbani,ni muda ambao watu walikua wanajificha kukimbia michango ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa ajili ya kupokea kidato cha kwanza. Lakini kwa sasa mambo yamebadilika Serikali inajenga vyumba vya madarasa kila sehemu kwa ajili ya kidato cha kwanza. Hatuna budi kupongeza na kuishukuru Serikali kwani tungekuwa tunachangishwa muda huu lakini sasa tunajengewa vyumba vya madarasa.”Alisema  

“Ilani ya chama cha mapinduzi imeweka bayana kuwa itaendelea  kuboresha na kudumisha mahusiano na mataifa mengine ili kufungua uchumi na kuwafuata wengine. Mheshimiwa Rais anatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi na ndio maana leo tunanufaika na miradi lakini kila siku tumekuwa tukipata wawekezaji katika sekta mbalimbali jambo litakalosaidia kuchochea uchumi na kuongeza ajira kwa vijana wetu”Alisema Ngole

Aidha wajumbe hao walishauri miradi ya UVIKO inayotakiwa kukamilika kufikia desemba 15  2021 kuhakikisha kuwa inakamilishwa na kuzingatia ubora uliokusudiwa bila kulipua.

Katika kuunga mkono jitihada za Wananchi katika maeneo inapotekelzwa miradi ya maendeleo Ngole ameahidi kutoa mifuko 250 ya Saruji na miche 300 ya parachichi kwenye maeneo yaliyopitiwa na Wajumbe hao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Njombe Kissa Gwakisa amewashukuru wajumbe wa kamati hiyo kwa kuunga mkono kufanikisha utekelzaji wa miradi hiyo na ameahidi kuendelea kusimamia utekelzaji wa ilani katika wilaya na kuhakikisha kuwa miradi inakuwa bora na yenye tija kwa jamii.

Ziara hiyo iliyogawanyika katika makundi manne iliweza kuzifikia Halmashauri zote za Mkoa wa Njombe Ikiwemo Ludewa,Makete,Wang'ing'ombe na Wilaya ya Njombe ambayo imeundwa na Halmashauri tatu ikiwemo Halmashauri ya Mji Makambako,Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji Njombe.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe