• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WITO WATOLEWA KWA WATENDAJI KUWAFUATILIA WAJAWAZITO NA WATOTO WANAONYONYESHWA

Tarehe iliyowekwa: November 18th, 2024

Na,Ichikael Malisa .


Watendaji wa kata za Halmashauri ya Mji Njombe wametakiwa kuendelea na Kampeni ya lishe ,kwa kuhimiza lishe bora kwa wajawazito na watoto wachanga na  kuhakikisha watoto wananyonyeshwa kikamilifu kwa kipindi cha siku 1,000 za mwanzo, ili kupambana na changamoto ya udumavu.


Wito huo umetolewa Tarehe 18 Novemba 2024 na Mkuu wa Wilaya ya Njombe,Mhe.Kisaa Gwakisa Kasongwa katika kikao cha tathmini ya utekelezaji wa viashiria vya mkataba wa lishe kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2024.


"Tumepiga hatua kubwa katika jitihada za kupunguza udumavu,nimeona kampeni zinafanyika ,siku za afya na lishe,tulizungumza hapa suala la kuwafuatilia wajawazito na akina mama wanaonyonyesha ni muhimu sana,lazima tuendelee nalo kwa bidii tisiache ,tuhakikishe tunabaki kuwa na alama ya kijani"Alisema.


Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Njombe Dkt.Jabil Juma alitoa msisitizo kwa watendaji kuendelea kufuatilia lishe za watoto shuleni kwa  kuhakikisha kila shule wanafunzi wanapata chakula chenye virutubisho vyote sambamba na kuhimiza uwepo wa bustani za mboga mboga.


Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi.Fransisca Mosha aliwasisitiza watendaji hao kuwafuatilia wajawazito kwa karibu ili kupambana na changamoto ya watoto wanaozaliwa na uzito pungufu ambao wamepungua kutoka asilimia 10.2 hadi asilimia 8.56.


"Niwaombe watendaji tusimame kidete na wajawazito tusiwaache  ili kupambana na changamoto ya watoto kuzaliwa na uzito pungufu.Tumepiga hatua lakini bado."Alisema.


Naye Mdau wa Lishe kutoka mradi wa USAID Lishe Projact Bi.Lilian Kipeta ,ametoa rai kwa watendaji kuendelea kutoa  elimu sahihi  ya lishe kwa akina mama pamoja na kuadhomisha siku ya afya na lishe kama mwongozo unavyotakiwa kwa kuhakikisha jamii na wataalamu wote katika kata wanashiriki kikamilifu.


"Njombe mnafanya vizuri ,inatia moyo,jitihada hizi ziendelee na sisi tupo nanyi bega kwa bega ,kikubwa tuhakikishe tunawafuatilia waliogundulika kuwa na changamoto ili wasiwe sababu yakuturudisha kwenye alama nyekundu."Alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe